HAPPY 4YRS ANNIVERSARY YKM


TAREHE KAMA YA LEO 23/09/2012 YKM (YOUTH KINGDOM MINISTRIES) ILIZALIWA.
FOUNDER WA HUDUMA HII NI PASTOR RAPHAEL JOACHIM LYELA.
HIVYO LEO TUNAADHIMISHA MIAKA MINNE YA UWEPO WA HUDUMA HII.

YKM ni kifupi cha Youth Kingdom Ministries.

Huitwa Ministries kwa sababu ndani yake kuna huduma (Ministries) tisa.

YKM  ni huduma ya vijana na inaendeshwa na vijana. Huduma hii haifadhiliwi na mtu yeyote zaidi ya members wake wenyewe.

Huduma hii haipo chini ya dhehebu lolote bali ipo na inatumikia ufalme wa Mungu.

Mwanzilishi wa huduma hii anaitwa Raphael Lyela na anakaa Dodoma kwa sasa. Wengi wetu humwita daddy!


KUSUDI LA KUWEPO YKM

“Kuwafanya vijana kuwa wanafunzi wa Yesu Kristo kwa kuwafundisha Neno la Mungu ili wapate ufahamu sahihi utakaowasaidia katika maisha yao ya sasa na ya baadae kwa ajili ya utukufu wa Mungu na Ufalme wake”

MAONO YA YKM

“Kuwa chombo kinachoaminika kwa kuwafikia na kubadilisha mfumo wa fikra wa vijana ili uwe sawa na Neno la Ufalme wa Mungu kwa ajili ya kuleta mabadiliko na matokeo katika familia, jamii na taifa kwa ujumla na kwa utukufu wa Mungu ”

HUDUMA ZA YKM

1.Mindset Upgrade:(Empowered for transformation,Romans 12:1-2). Uhusika na kubadilisha mtizamo wa vijana kwa kutumia neno la Mungu.

2.Kingdom Transformers: (Leadership that transforms,Acts 17:6) Uhusika na kuandaa viongozi katika Nyanja mbali mbali za maisha.

3.The Bridge is Today:(Shaping your destiny today,Proverbs 12:1).
Uhusika na kukutoa katika ulicho fanya zamani na kukuonesha waweza fanya nini  ili uwe na future nzuri.

4. Kingdom Worship:
(His presence,my destiny;John 4:23) Uhusika na kutuongoza kumwabudu Mungu kwa usahihi.

5.  Kingdom Charity:
(Impacting through giving;Acts 20:35)
Uhusika na kuwafikia wahitaji.

6. Kingdom Ladies:(Ladies with value,Ezra 9:2):Uhusika na kuandaa wadada watambue thamani yao.

7.Gospel Corner:
(Youth to Jesus.Youth in Jesus.Youth in Jesus, Mathew 28:16-20).
Uhusika na kuwafikia watu na injili ya wokovu.

8.Kingdom Gents:
(Performance1Kings 2:2-3, Col 1:14 & Psalm 125):Uhusika na kuandaa wanaume watakao yatambua na kuyasimamia majukumu yao ya kiume.

9. Kingdom Inspiration:
(Inspired for influencing generations,   Isaiah 41:6-7): Uhusika na kuinua mioyo ya watu kwa kuwatia moyo kwa misingi ya neno la Mungu.


Huduma hizi zote zina viongozi

YKM MIKOANI

YKM inafikia mikoa ifuatayo mikoa ifuatayo kwa sasa:

Ruvuma, Dar, Arusha, Mwanza, Iringa,Mbeya, Kilimanjaro, Dodoma ,Morogoro na tunazidi kuelekea kwenye mikoa mingine kadri siku zinavyoendelea.

Kila mkoa una uongozi wake wa viongozi Kumi.

UTENDAJI WA YKM

YKM inawafikia vijana na mafundisho kwa njia ya:

1. Simu zao ( SMS na Whatsapp)

2. Kwa njia ya mtandao Tovuti na Facebook
(http://www.ykmjesusup.org/ and  https://www.facebook.com/YouthKingdomMinistriesJesusUp )

3. Kwa njia ya Events mikoani mwao.

Mikoa iliyotajwa hapo juu ina whatsapp grups unaeza unganishwa kama upo whatsapp.

Kwa taarifa zaidi tembelea tovuti yetu: http://www.ykmjesusup.org/

MAJUKUMU YA MWANA YKM

Members wa YKM wanamajukumu yafuatayo.

1.Kusambaza message za YKM ili habari njema iwafikie watu wengi zaidi.

2.Kushirikiana na members wenzako kuipeleka injili ya Kristo kwa kipaji chako na hata mali zako.

MANUFAA YA YKM KWAKO

Utapata manufaa yafuatayo:

1. Utakua kiroho

2. Utapata platform ya kumtumikia Mungu

3. Utapata familia kubwa sana ya vijana wenzako watakao kupenda na kukujali kwa dhati

4. Utakua pia katika Nyanja nyingine za kibinadamu (holistic human development)

5. Nk.

This is a brief about YKM, utazidi kuifahamu huduma kadri utakavyo jihusisha nayo.

Maoni