NAFASI YA ROHO MTAKATIFU KATIKA MAHUSIANO YA KIMAPENZI.


 By Raphael JL:

Kwenye mahusiano,kama nilivyosema kwenye somo lililopita, yako mengi yanayochosha sana na hasa kama haujasimama na Mungu na kuwa na utulivu wa ndani wa kusikia na kumsikiliza Mungu anavyosema na kukuongoza kupitia mawazo,fikra na hisia zako kufanya uchaguzi wa mke au mume ajae. Nilisema kwenye somo la nyuma kuwa haijalishi mmekutana wapi au mtumishi gani KAKUPIGIA PANDE,lisije likawa pande la msumari kooni, ila sasa nataka niendelee na sehemu ya pili na kubwa sana,kaa mkao wa kujifunza.

UNA UHAKIKA? Je, ukiulizwa leo, kama una uhakika na mtu uliye naye utasemaje? SIO LAZIMA UKOSEE KOSA LA BABA YAKO KAMA ISAKA NA YAKOBO,ila unaweza kuchagua mwenyewe kutegemeana na hali unayokuwa nayo. Umekutana na mtu kwenye gari,au kwenye huduma, au kwenye mamtatizo au alikuwepo akikutia moyo wakati umefiwa na wazazi na mwisho mkajikuta mko connected...ni kweli kuwa something has to connect you to someone...whatever connect you to someone will sustain you or break you...sasa hapo ndo tupaangalie leo na kuona nafasi ya ROHO MTAKATIFU...kwenye mahusiano hayo hayo...hii ni kuepuka maumivu ya makusudi na kujitakia...kumbuka SUKARI HAIWI CHUMVI KWA KUICHANGANYA NDANI YA ASALI....

KIWANGO CHAKO CHA KUMJUA:Roho Mtakatifu hasemi uongo wala hadanganyi ila sisi tunajua yeye ni msaada wetu, mshauri wetu na pia mwalimu wetu.Wote waliomtegemea hawajajuta.Mfano, mkaka kamfuata mdada na gear ya BWANA KASEMA,mdada kwakuwa alikuwa anasubiria sana hiyo nafasi anakubali kwa sauti ambayo hajaisikia yeye mwenyewe,anamwaga moyo wake na kuamini yaani kama Bwana kasema itakuwa lazima niwe hivo tu...so wadada wengi wamejikuta wanaingia KICHAKANI kwa kudhani hivo tu yatosha...fahamu kuwa kichaka kina vitu vingi sana ambavyo usingependa kuviona au kuvijua....

DONT ABORT THE PROCESS:Roho Mtakatifu yupo na anatusaidia mengi tu, nakubali kuwa Mungu anaweza kuzungumza kwa njia yoyote ile na hata sasa najua anasema, na najua yapo mahusiano ambayo kabisa Bwana alisema na ikawa ndo kasema hivo moja kwa moja...lakini kwasababu ya kutokumjua na kumsikiliza ROHO WA MUNGU vijana wengi wamekuwa WANAHARIBU MCHAKAKATO...ni hatari sana kujikuta umeolewa na mkwe wako na sio rafiki yako...kumbuka urafiki unatengenezwa.....sasa ndo nasema hivi hapo....USIHARIBU MCHAKATO....hata kama Bwana kasema inabidi umuulize kama ndo kakwambia uende ukamwambie muhusika kwani kwa kukurupuka kwako unaweza ukajikuta UMEHARIBU MCHAKATO.....friendship is a function of social UNGAPPING...so ukianza na ishu zako za kiroho from point A unaweza ukajikuta umoa au umeolea na kitu ulichokuwa unakiogopa kwa miaka mingi...ni hatari sana....

WASAIDIZI WA ROHO MTAKATIFU: Walipowaona mnaimba pamoja, mnakula pamoja, mnatembea pamoja, mna huduma inayofanana, mna sura zinazofanana, mnatokea mkoa mmoja na hata mna kabila moja...basi wakaibuka manbii 400 wa BAALI ambao wakaanza kuwafananisha na kuona nyie mnafanana hakika na inawapasa kuoana...na nyie kwa KUJAA MAJI mnaanza kutengeneza mazingira ya KUUTIMIZA UNABII WA MFALME KORESH,laiti kama ungejua kuwa MAISHA YA NDOA ni ya watu wawili na Bwana Yesu katikati...mkishaona mtagundua haha hahaha heee KUMBE HATA HAMFANANI...umeoa mke wa mtu mwingine...umeolewa na mume wa mtu mwingine...umelazimisha.....NAFASI YA ROHO WA MUNGU HAPO IKO WAPI? Sikatai kuwa Mungu anaweza kuwatumia watu kutukutanisha na watu wetu sahihi...ila USAHIHI WA HAO WATU TUNAUPATA WAPI? NI HATARI SANA KUUTEGEMEA UPEPO.

Kama humuamini Roho Mtakatifu basi hilo ni tatizo la kipekee sana,maana utaendelea kutibu vidonda mpaka uchakae...kimsingi Roho wa Bwana yupo na anafanya kazi....sema kuna wajinga fulani wamekuwa wanatumia vibaya na kumsingiziia na kumbe ni hisiaa zao from ISIDINGO...na ndo maana mwisho wa siku inaonekana kama Roho Mtakatifu hayupo na hafanyi kazi lakini kimsingi ni UKIROHO WA WAROHO WACHACHE tuuuuu...
Ndio...yaani unaoa na kuolewa na mtu wa kulazimisha au kudanganywa na kisha unaingia nae ndani na unaona kama vile unaishi na mkweo...yaani huna uhuru...yaani huna amani na unaona kabisa...yaani unashuhudiwa kuwa ulichemka kabisaaaaaaa na unaiona waziwazi....unatamani ufe na hufi...unatamani na kuomba afe na hafai MPAKA MMELIPA GHARAMA YA KUHARIBU MCHAKATO...hapo ni kama umeoa mkwe vile...utatamani uchelewe kurudi home ili ukute amelala....vyvote itakavyokuwa yaaani ila utajiona tu ni kama UMEVAA NGUO ZA JESHI NA UNAENDA KUOGELEA....


VITISHO VYA KIVULI USIKU: Mungu yupo na anaweza kukusaidia kuvuka hakika, ila sasa unajikuta unakosea maana una haraka ya kuolewa au kuoa maana unaona umri unaenda, unajiona umeanza kuwa mzeee fulani hivi, unajiona mwili wako unaanza kupoteza mvuto wa kisichana, unajiona unajinenepea tu na hupendi, unajiona tu unahamu sana ya kuwahi KUOLEWA NA KUOA na mwisho kumbe ulikuwa unawahi KWENYE SHAMBA LA MBIGIRI NA UKO PEKU...WENGINE WANATAKA WAWAHI KUOLEWA na kuoa ili wazae mapema...haha hahah hah kazi kweli...so mwisho wa siku wanaoelwa na kuoa halafu wanagundua hawazai maana UWEZO WA KUPATA MTOTO hauko kwenye haraka za kuoa na kuolewa..ila sasa unafanye...na ikitokea umezaa basi unawafanya watoto wako kuwa wapenzi wako kwani hupati UNACHOSTAHILI, yaani unapata ULICHOTAKA ambacho ni watoto...ni hatari sana KUKIMBILIA USIKOJUA...UTAJIKUTA UMEKUMBATIWA NA MTU KAVAA KOTI LA UPUPU....

Maoni