YKM DAR ES SALAAM - KINGDOM CHARITY AT MSIMBAZI MATERNITY CENTER
Kama ilivyo moja kati ya huduma tisa (9) zilizopo ndani ya YKM ambayo
ni KINGDOM
CHARITY yenye kauli mbiu isemayo
Impacting through giving/ Kubadilisha maisha ya jamii kupitia utoaji. Hii
inapatikana katika kitabu cha Matendo ya
Mitume 20:35.
“35 Katika mambo yote nimewaonyesha ya kuwa kwa kushika kazi hivi
imewapasa kuwasaidia wanyonge, na kuyakumbuka maneno ya Bwana Yesu, jinsi
alivyosema mwenyewe, Ni heri kutoa kuliko kupokea.”
KINGDOM CHARITY inahusika na kuwafikia na kuwagusa wahitaji
mbalimbali katika jamii na kuwaonyesha upendo wa Mungu kupitia utoaji.
Mnamo tarehe 12/01/2017 siku ya Alhamisi YKM DAR ES SALAAM ilifanya
tendo la Upendo kabisa yaani CHARITY katika kituo cha kulelea watoto wasio na
wazazi (au mzazi mmoja) cha MSIMBAZI
MATERNITY CENTER. Kituo hiki hulea watoto kuanzia siku moja mpaka miaka
mitatu, na baada ya hapo huamishwa kituo kwa ajili ya malezi zaidi. YKM DAR ES SALAAM
ilipata kibali cha kutoa msaada/sadaka ya vitu kama sukari, sabuni, biskuti,
mafuta na kwa kiwango kikubwa Pampers pamoja na maziwa ya lactogen kwa kuwa wengi
wao ni watoto wadogo sana. Vitu hivi walivikabidhi kwa wahusika na kupokelewa
kwa furaha.
YKM DAR ES SALAAM walipokelewa
vizuri na kutambulishwa pia kuonyeshwa mazingira ya kituo hicho ambapo walipata
fursa ya kupiga picha na kucheza na baadhi ya watoto wale wenye umri wa kati
yaani chini ya miaka mitatu.
YKM DAR ES SALAAM pamoja na watoto wote pia walipata nafasi ya
kusherehekea kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa yaani BIRTHDAY ya dada Nyarobi Nkwimba ambaye alitimiza miaka
kadhaa siku hiyo. Dada Nyarobi aliona ni vyema kwenda kusherehekea pamoja na
watoto hawa kama moja kati ya jambo la kuwafurahisha na kuonyesha upendo kwa
watoto hawa.
Mwisho ni Shukrani za dhati kwa Kiongozi wa charity mkoa wa Dar es
salaam Ndugu TOP KASORO kwa maandalizi mazuri aliyoyafanya na kufanikisha tukio
hili ambalo kwetu ni agizo la YESU mwenyewe. Pia shukrani kwa wale wote ambao
walijitoa katika kuwawakilisha YKM DAR ES SALAAM, ambao ni
1. VIOLETH BURA
2. JULIETH WINSTON
3. STEPHEN MUNISS
4. ELIBARIKI KIVUYO
5. PRAYGOD SARAKIKYA
6. REBECCA YONA
7. NYAROBI NKWIMBA
8. EMANUEL AMON
9. KELVIN DANFORD
10. REINA HEPELWA
11. ANNA TUPA
12. RONALD FOYA
13. GRACE MASANJA
14. UPENDO SENI
15. GWAMAKA MWASOMOLA
Tujitoe katika kumtumikia Bwana
MUNGU AWABARIKI
MUNGU IBARIKI YKM
2017_USHIRIKA_NA_MUNGU
Maoni
Chapisha Maoni