Ads Top

CLOSET PRAYERS TESTIMONIES (From 18th-19th August 36Hrs)




36 HOURS CLOSET PRAYER
AUGUST 18-20TH 2017
THEME: REPOSITIONING YOURSELF
TESTIMONIES
ROSEMARY
Namshukuru Mungu sana kupitia  mtumishi wake na nyie wote humu mmenifanya nione umuhimu wa kumrudia Mungu. Nina amani sana rohoni mwangu.Namuomba Mungu anisimamie katika safari yangu hii mpya ya kumtegemea yeye tu. Asante Mungu kwa kuniokoa mimi mdhambi. Asante sana dad kwa upendo wako na uongozi wako mpaka mimi mwenyewe kwa hiari yangu nimeamua kuokoka. Mungu atubariki sote na atuongoze.

GRACE MAPHIE
 Namshukuru Mungu kwa maombi ya jana nimemwona hakika pia naendelea kujifunza Daddy ubarikiwe.
Naendelea na maombi ya kurudi kwenye nafasi lakini namshangaa huyu Mungu jana nimeweza kufanya jambo ambalo hapo nyuma nilikuwa nafanya kwa kusuasua yaani jana sio kwa huo upenyo niliouona nalibariki jina la Mungu wetu

HILALIA PHILIPO
Jana wakati naingia kwenye maombi ya Toba ni kama nililetewa CD ya maisha yangu ya mwanzo NILIPOANZA WOKOVU. Nikawa naona nilivyokuwa MOTO WA KUOTEA MBALI. Nikakumbushwa mambo mengi ambayo nilijikuta mimi JINGA KABISAAAA NILIIKUWA NIMEKUBUHU. NIKAOMBA MUNGU ANISAMEHE. DAH until NOW bado naona ule mda wa Toba hautoshi aisee. Yaan naona nilipotoka kwenye nafasi yangu yaani kama nilipanga nafasi ambayo iko mbali. Kurudi inahitaji GHARAMA  KABISA. Na nashukuru MUNGU kadri navyoendelea kuomba Toba ndo kadri navyoendelea KUPATA  AMANI ZAIDI. Yaani natamani tuendelee mpaka SIKU YA UNYAKUO AISE.
Nawaza mambo mengi mpaka NAKOSA NENO LA KUMPA MUNGU KAMA SHUKRANI NA KUNIPA UFAHAMU HUU AMBAO HATA MAKANISANI KWETU SIJAWAHI KUSIKIA.
Aisee. Kwanza hata style ya maombi imebadilika. Kuna wakati nilikuwa nikiomba yaan hata sielewi nimesema nn. Dah yaan i dont know how to say to God. Am SPEECHLESS
QUEEN FLETCHER
Namshukuru sana Mungu kwaajili ya jion hii...Kila Mara nikiona shuhuda mbali mbali I was wondering mimi mbona sielewi elewi bado... Well Mungu amenifungua. Amenifunulia majibu jion hii. Amenionyesha how much wrong I was in my life and live out of my position for so Long. Thinking that I was right...Roho mtakatifu kanichimbua yale yaliofichika.
Nimejikuta nacompare with what dad was teaching us nikawa nalia tu.In short I was thinking the way Am living is right and that how it's supposed to be... lkn baada ya kufunguliwa nimejiurumia mimi. Namshukuru sana Mungu anaeendeleakunifanya mpya. I feel so good now. Namuomba Mungu akamilishe kaz aliyoianza. I want the whole package in Jesus name
Yaan NANG'ANG'ANA!
God is good
This is my Testimony.

ELIZABETH KING
Ngoje niseme ukweli tu, hivi unajua ninaomba kwa raha sana situmii nguvu wala sijikakamui wapendwa, unajua maana navyokaguliwa na kukumbushwa mahali nilipoangunga, na natubu ilo eneo nalokumbusha najihic mwepesi sana, halafu naomba kwa utulivu wa hali ya juu, mtaa huu unakelele but si kwa utulivu  huu nilioupata, jamani si kwampangilio huu wa hoja zenye nguvu hadi nakaa najiuliza hii aina ya maombi ya namna hii ni mimi naomba au jamani dah nashindwa kuelezea wapendwa...
Unajua nini huku kutoka kwenye nafasi kulinifanya mpaka nikiwa nataka kusoma neno la Mungu moyo unanipasuka wapendwa yaan kama nimekutana na el- shababu, yaan mwanzo nilitamani hata kutofanya haya maombi, coz nilikuwa naona kila kitu baba alichoongea kama ndo kinanivuruga zaidi, nikawa nasema hivi mbona hali kwangu ni mbaya saana na ndo kwanza giza linazidi kutatanda...
Yaan nimekaa hvy hvy kwenye group kishingo upande huku nikijiandaa kuingia kwenye maombi ya jujikakamua, na mara nyingine hata uelewi unachoomba, miayo mingi yaan fujo tu.... ila jamani mwacheni Mungu aitwe Mungu cku moja kabla baba ajasema anataka kuwapunguza watu wasiochangia nikaanza kupitia somo ili alilofundisha taratibu, sasa ndo nikalipenda na nikapata hamu ya dhati kutoka moyoni kulifuatilia na ndo mwanzo wa mimi kuanza kuelewa yaan kupata ufahamu wa hiki alichotufundisha....
Jamani nikisema kurejeshwa kwenye nafasi, kutakaswa, kufunguliwa fahamu, kutulia madhabahuni kwa Bwana, na kusoma neno na ukawa unalielewa raha, jamani na maanisha nachosema, ni maombi yangu ya mara ya kwanza kabisa kuona Mungu anajibu maombi kwa haraka namna hii, kweli c kila neno linalosema nakuaminiwa na watu wengi lakuliamini jamani Mungu ajibu maombi mpaka badae kesho tu nk, lkn Mungu anajibu maombi hata wakati huo huo,  Mungu ni mwema kwangu jmn...

JUSTINE YOMBO
Bwana Yesu asifiwe wapendwa, namshukuru Mungu kwa kuniunganisha na mtumishi wa Mungu @RaphaelJL, kupitia maombi haya nimeuona mkono wa Bwana. Najisikia wepesi ila Mungu amefanya zaidi ya hapo. Baba ulisema Jumatatu tukafanye kazi mimi ntaenda kufanya kazi Jumatatu. Wapendwa ukiwa nje ya nafasi yako baraka zako haziwezi kukulocate. Kila kitu kinacho kuhusu kipo kwenye nafasi yako. Sina mengi zaidi. Namshukuru Mungu kwa progress hii. Haya maombi ni mpango wa Mungu kuturejesha mahali sahihi.

AMINA MNZAVA
Nina ushuhuda mkubwa Mimi nimepona jamani uwiii, nilikuwa natengeneza Na mpenzi wangu nilinunua La plot na nikaanza kujenga bila kumwambia, nimetengeneza jamani maana mahali tulipokuwa tumefika khaaa pa bays asante Mungu kwa kuijua nafasi yangu kama.msaidizi nimerudi mwanampotevu. Tumepona ndoa yangu imepona Jina lake libarikiwe

GRACE MAPHIE
Namshukuru Mungu kwa neema na rehema zake hakika nimemwona kwa namna ya ajabu we Mungu ni mkuu hakuna aliye kama wewe matendo yako bhana siwez kueleza.

MRS. CELINA MAGIGITA
TWEKA MPAKA KILINDINI. SAMAKA WAPO, ISSUE NI KUSIKIA BWANA ANASEMA NINI...TWEKA MPAKA KILINDINI
4 Hata alipokwisha kunena, alimwambia Simoni, Tweka mpaka kilindini, mkashushe nyavu zenu mvue samaki.
6 Basi, walipofanya hivyo walipata samaki wengi mno, nyavu zao zikaanza kukatika;  (Luka 5 :4, 6)
Shalom wana wa mfalme!
Ninarejea msisitizo wa Mchg.  Tweka mpaka kilindini!
NILICHOSIKIA KWA BWANA MASAA YA MWISHO KATIKA KUHITIMISHA MAOMBI YA KURUDISHWA KWENYE NAFASI.
HISTORIA YANGU YA UFUGAJI.
2008 nilianza rasmi ufugaji nikiwa nafugia nyumbani kwangu. 2010 Bwana alipanua hozi yangu nikajieneza na kupata shamba Miyuji, nikajenga mabanda makubwa ya kutosha kuku 2,000 kwa mara moja. Nikahamishia mradi huko baada ya kujenga kiwanda kidogo cha chakula cha mifugo na nyumba ya watenda kazi. Nikaweka kuku 2,000 hali ikawa nzuri sana kwa wiki nikawa nauza tray za mayai 400 Kibaigwa na soko kuu la majengo kwa wauzaji wadogowadogo. Ibilisi hachezi mbali aliingia kupitia mtoto wa wifi yangu akaniibia sana nikaishia kuufunga huo mradi mwaka 2015.
Dec 2016 mume wangu akanitia moyo nikainuka tena nikaanza kufuga nikaweka kuku wa nyama (chotara)  1,000. Wakaenda vizuri kwa muda mwezi Februari ghafla mdondo ukawaingia wakafa kuku 600 ndani ya wiki moja. Tangu wakati huo nilikata tamaa kabisa kufuga nikaplan kubadili matumizi ya hayo mabanda kwa kuwa wiki ijayo nitaanza mradi mpya wa kukoboa,  kusaga na kupaki sembe nikawa nimepanga nitayageuza yawe maghala ya kuhifadhia mahindi.
Usiku nimemuomba Bwana aseme nami neno katika kuhitimisha maombi, nikautuliza moyo wangu kwa Bwana pasipo kuwazia kabisa ishu ya miradi wala biashara maana nilishafikia maamuzi ya kufanya sembe na duka la mavazi tu, hivyo hilo eneo la kazi za mikono sikuwa na mzigo wa kuliombea kabisa kwenye hizi siku 3 in fact sijagusa kabisa kuombea biashara, siku zote nimekomaa na matengenezo na kurudishwa kwenye nafasi tu.
NILICHOSEMESHWA KWA NDOTO!
Usiku wa leo mida ya alfajiri ya saa 10 nimeota ndoto hii.
Nimeona katika ndoto niko natembelea mradi wa kuku wa nyama na mayai wa mama 1 ana kuku wengi sana. Nikamwambia nimekuja unielekeze mtu sahihi wa kuniuzia vifaranga ili nikafuge. Akanitajia wauzaji 2 mmoja ni mtumishi Pallangyo nikamwambia nitachukua kwa Mtumishi Pallangyo kwa kuwa ninamfahamu.Nikastuka ndotoni.
NASISITIZA HATA KUWAZA TU KUKU SIJAWAHI KUWAZIA!
Binafsi nimemshangaa sana Mungu. Huu ni urejesho wa aina yake naiona Zaburi 126: 1 imekuwa halisi kwa hiki cha leo!
"Bwana alipowarejeza mateka wa Sayuni, Tulikuwa kama waotao ndoto". (Zaburi 126 :1)
Ninamshangilia na kumfurahia Bwana kwa matendo makuu aliyonitendea kupitia hii programu.
MUSA JOSEPH
Kipekee namshukuru sana Mungu kwanza uombaji ni lazima ubadilike...Ukipata ufahamu kuomba kuna badilika sana jamani.
IMEKUWA DHAHIRI KWAMBA MUNGU AMENIREHEMU NA AMENIFUNGULIA MILANGO AMBAYO HAKUNA AWEZAE  KUIFUNGA.
Barikiwa Dady.. Ninakupenda sana.
MUNGU WA MBINGUNI APOKEE SIFA ZOTE NA UTUKUFU..  HAKIKA AMEFANYA JAMBO KATIKA MAISHA YANGU.
Semina ya jana... Na leo pia ninaendelea kupata mkazo wa Waefeso 6:10-18
MUNGU NA ANISAIDIE KATIKA KUUTENGENEZA UFAHAMU WANGU...


ESTER WILLIAM
Kwakweli Mi namshukuru Mungu ktk maombi haya, kwanza kabisa shetani alikuwa amejiinua kwangu kuhakikisha sifungi,ijumaa nimeamka kidole cha mkono kinaniuma sana kilikuwa kimeanza kidogodogo kuvimba nikaamka kimezidi sana nikaenda hospitali wakakipasua nikarudi na maumivu makali nilipewa na dawa za kumeza, nilichofanya nikasema hapa sinywi dawa yoyote hadi jumapili, ndo takunywa, nilishauriwa na nispo kunywa dawa kitaoza nikajibu dawa nitakunywa ila jumapili, nilichekwa na kuambiwa nyie walokile mnakazi kwani Mungu hajui kuwa unaumwa? ila nashukuru ndivyo ilivo kuwa.
Nashukuru najiona nina badiliko kubwa ndani yangu, hasa likutamani niongee na Mungu kila saa, nipo tofauti na nilivyokuwa,Mungu akubariki saana Pastor kwa maono haya umetupa kusimama ktk nafasi tulizotakiwa tuwepo.
Jana napo shetani kainua vita juu yangu, kuna binti wa kazi, nilikuwa nimebaki nae,ana umri wa miaka17, ilikuwa yupo karibu kuondoka kwao anakaa dodoma kuna baadhi ya hela yake alikuwa anaisubiria, nikamwagiza mboga mda wa saa 4 asubuhi, kaenda jumla hajarudi hadi sasa, ila najua hiyo itakuwa ni roho chafu iliyopo katika hii nyumba, maana historia iliyopo ndiyo hiyo zaidi ya mabinti wa4, wanaondoka kwa stahili hiyo, nitahakikisha nasimama katika nafasi yangu kuiteketeza hii roho, nakuhakikisha kujua huyu bint alipotorokea na arudi aje aondoke kwa amani, nimekuja tu mara moja dar kwa mama wa hiyari ndo yanatokea baya naamini Mungu amenileta kwa makusudi mahali hapa lipo kusudi lake huruhusu yatokee haya.


MUSA JOSEPH
Esfeso 6:10-18
10 Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake.
11 Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani.
12 Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.
13 Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.
14 Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,
15 na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani;
16 zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.
17 Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu;
18 kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote;
Katika mlolongo huo maombi huwa ni ya mwisho. Cha kwanza ni silaha ambazo zitapatikana kutokana na ufahamu sahihi.
Kupingana na hila za shetani ni zaidi ya maombi ni lazima kwanza uwe na ufahamu wa silaha zote.
Kuna watu wanaomba sana na hawapat majibu ya maombi yao.
Kwanza ni lazima kuwa na ufahamu sahihi wa kitu gani unakiombea..
Mungu anayejibu maombi huangalia usahihi wa maombi na sio wingi wa maombi na kinachofanya maombi yajibiwe ni kiwango cha nguvu kilicho ndani yako.
Ili uombe maombi ya muda mrefu kwanza unahitaji ufahamu sahihi then nguvu ndani yako.
Ni kitu kibaya kuwa na ufahamu usio sahihi na kwenda mbele za Mungu.
Maana yatakuwa ni maombi ya mpumbavu..
Ukizielewa silaha zote zilivyo hapo ndipo hata maombi yataenda sawa.
Uhodari katika Bwana hauji kwenye maombi, uhodari unatengenezwa kwenye mchakato... So ninlazima kuwa na ufahamu sahihi wa Neno la Mungu.
Shetani ni tofaut na mapepo, hakemewi akatoka yeye ni mkuu wa nguvu zote za giza..yeye tu ndo anauwezo wa kutokea mbinguni.... Shetani anatolewa kwa ufahamu sahihi.
Ufahamu ndio unaomkemea shetani.. Kama hujui kweli kwenye eneo husika huwezi toka.
Mathayo 4:1---
Yesu alikuwa na ufahamu na ndo maana alimshinda ibilisi.
Usiingie kwenye maombi kama hujavaa silaha zote...

FRANK MTAHA
Kibinafsi namuona Mungu sana katika mambo mengi mno.
Kwanza nimekuwa mwepesi sana wa kuomba kwa kiwango kikubwa, pili amani ya ndani imeongezeka maradufu na kuna mambo aambayo nalikuwa na hofu nayo kwamba sitafanikiwa lkn sasa hivi moyoni mwangu ninasema HAKUNA JAMBO GUMU MBELE ZA MUNGU, tayari nimefanikiwa moja tena katika kusema tu kwamba hii ni milki yangu na kweli imekuwa.
Kwenye huduma leo ndipo Mungu alipojidhihirisha kabisa ubaarikiwe pastor kwa somo hili na utaratibu mzuri wa maombi ulioongozwa na Roho wa Bwana,Mungu ni mwema sanaa

SAINA KITTA
Jaman nashindwa hata nisemaje maana nimemuona mungu kanifungua kabisa , mpaka najiona mwepesi mungu azidi kukupa maono mtumishi wa Mungu

AMINA MNZAVA
Jamani ni shuhuda kwa kweli nilipoamka asubuhi nikiwa nimekaa nikapata wazo la kuanzisha huduma ya wanawake inaitwa WOMAN of GLORY, sijawahi kuwaza hii heading naamini Bwana aliyeanzisha kazi hii ataikamikisha utukufu kwa Mungu.


CONCESA SHUBIRA
God's mercy has been shown unto me during this prayer season. Finding my position and being re-stablished in Him through the prayers and actions has brought me nearer to the Lord. This journey has been a revealing one for me. Meditating upon the word each day and learning that there is more in my life that God has planned for me,  and not only what i know. I can brag and say that Jesus has done it again!!!
He is a wonderful and merciful God.
Thank you daddy for this sesion am grateful to have you.
Stay blessed everyone!!

DOREEN KIARRA
Maombi haya hakika hayakuwa ya kawaida.  I am tooo blessed...  , na shuhuda zazidi kunibariki pia.  Mungu wetu asikia na ajibu. And He moves instantly

MRS. CELINA MAGIGITA
USHUHUDA WANGU
Utangulizi:-
Mnamo Tarehe 10/08/2017 nilijiunga rasmi ndani ya hii Safina. Kupitia rafiki yangu mpenzi Mrs Amina Myombo.
Nikajitambulisha hivi:-
Mrs Celina Magigita. Nimeokoka, mfanyabiashara, kihuduma ni mwalimu na mhubiri, ninaishi Dodoma. Nipo humu kwa nia ya kuvuka nilipokwama. Asanteni kwa ushirikiano. Nimesoma masomo kupitia dada Amina,  nimebarikiwa sana. Tupo pamoja ndugu katika Kristo Yesu.
Shauku na Nia yangu kuu kujiunga humu ilikuwa KUVUKA NILIPOKWAMA!.
Neno linasema:-
"Nawe utakusudia neno, nalo litathibitika kwako; Na mwanga utaziangazia njia zako". (Ayubu 22 :28)
Kusudi langu halikuwa kuja kufahamiana na watu au kushangaa bali nilikusudia KUVUKA. nilimaanisha nilichokusudia na nikadhamiria KUVUKA.
Leo hii ikiwa siku 10 ndani ya SAFINA ninazo shuhuda kuu 3 za matendo makuu ya Mungu naam na ya 4 iko njiani naitarajia kuipokea wakati wowote ambayo ndiyo muhimu zaidi kwangu.
Mambo niliyotendewa ni:-
1. Akili zangu zimefunguliwa nimeelewa ili kuishi maisha ya Ushindi jambo kuu ni kuwa na UFAHAMU sahihi wa hilo eneo. Kwa hiyo nimejipanga kulipa gharama kujaza moyo wangu maarifa ya kiungu ili nipate ufahamu wa kutosha kuishi maisha ya utoshelevu na ushindi huku nikilitumikia shauri la Bwana.
2. Asante Ujinga imeniondoka, nimetembea kwenye mateso ya kujitakia ndani ya ndoa yangu kwa zaidi ya miaka 17. Kupitia maarifa niliyoyapata humu nimeweza kufanya maamuzi magumu ya kukaa kikao cha masaa 3 na kuwekana sawa na mume wangu hatimaye tumerejea Eden. Hali haikuwa nzuri kama ni shimo basi adui alishaliweka tayari kunitumbukiza. Asante mchg. Raphael kwa kunivusha nisitumbukie.
3. Eneo la uchumi limekuwa na mapito mengi sana na sintofahamu za hapa na pale. Kwa neno la mwisho alilonipa Bwana kwa njia ya ndoto nilipokuwa nahitimisha maombi. Limetosha kunipa kujua BWANA ananirejeshea utukufu wa NAFASI yangu kiuchumi.
4. Eneo la Kiroho hili ni nyeti zaidi kwangu na sijaelewa kwa nini Mungu amelifanya kuwa la mwisho kukamilishwa muujiza wake!
Nimekuwa katika mapito magumu sana yaliyopelekea mahangaiko ya kutokuwa na mchungaji mmoja wa kunilea kiroho kwa muda mrefu na shida kubwa ilikuwa baba wa familia kutaka nibaki kwenye dini nami nang'ang'ana kutaka kumtafuta Mungu kiroho zaidi badala ya kujifungia kwenye kifungo cha dini na mapokeo ya dhehebu.
Juzi kwenye toba na matengenezo nilikaa na mume wangu nikafanikiwa kujieleza kwa msaada wa Roho Mtakatifu hatimaye amenielewa na kukubaliana na ombi langu la mimi kupewa uhuru wa mahali pa kuabudu kiroho.
Huu kwangu ni muujiza mkubwa sana lakini haujakamilika bado ndio kwanza nimeanza kuomba Mungu anipe mchungaji sahihi wa kunilea kiroho ikiwa ni pamoja na huduma na utumishi uliomo ndani yangu.
Bwana ameahidi,
"nami nitawapa ninyi wachungaji wanipendezao moyo wangu, watakaowalisha kwa maarifa na fahamu" (Yeremia 3 :15)
Suala si kuwa ndani ya kanisa maarufu, jengo zuri nk.... Muhimu kwangu ni ninalishwa nini na hicho ninacholishwa kinanipa maarifa na ufahamu wa kutosha kuishi maisha ya utoshelevu pande zote na yanayompendeza Mungu!
Kwa huyu mtoto wa 4 ni muujiza ambao haujakamilika nawiwa kusema haya kwa pst Raphael.
Petro alitekewa alipokuwa uweponi mwa Bwana akaishia kusema na tujenge vibanda vitatu.. ...nahisi kuna mambo aliona bado hayajapatiwa majibu akatamani waendelee kubaki mahali pale kwa muda zaidi ili apokee yote kwa ukamilifu wote.

OMBI LANGU.
Humu ndani sijui kama wote tumevuka kwa kuzaa vile tulivyoingia nanvyo ndani ya Safina na tumetosheka kwa vile tulivyofanikiwa kupush hata tukazaa.

Binafsi mtoto namba 4 hajazaliwa mkamilifu ni premature anahitaji kusaidiwa ili akamilika na leo ndio mwisho wa hii incubator nawaza peke yangu joto nililo nalo litatoshea kumkamilisha! Bado sijaliamini joto langu hivyo ninaomba extension ya muda atakaona unafaa mbeba maono pst Raphael ili mtoto huyu akamilishwe na kukamilisha ushuhuda huu muhimu kwangu kiroho.
Naomba hekima yako mtu wa Mungu na muongozo ikiwa nitapata kibali moyoni kwako.
Jambo moja ninajua hakuna mtu anayefanikiwa pasipo msaada wa watu wengine. Kwa hilo nilijifunza nimejifunza  kunyenyekea na kuheshimu mchango wa watu kwenye hatma yangu.
Mchg. Raphael umeongeza thamani yangu kwa kuniweka kwenye njia sahihi kuielekea hatma yangu ya utukufu. Ni maombi yangu Mungu akuinulie watu wakuu watakaokushika mkono na kuongeza thamani ya maisha yako hata uufikie ukamilifu wa hatma yako duniani.
Nawapenda katika wote Bwana. Mmefanyika baraka kwangu kwa hizi siku 10, niliomba ushirikiano nilipoingia humu, namshukuru sana Mungu kwa ajili yenu kwani mmenipa ushirikiano mkubwa na kunirahisishia kupokea kwa kasi ya ajabu.
Barikiweni,
Celina.

IRENE JORAM
Namshukuru Mungu kwa haya maombi, na kwa ufahamu niliopokea kuhusu Nafasi yangu na jinsi ya Kusimama.
Binafsi, nmekua nikipitia katika kipindi cha kutamani kuyarudia matendo ya kwanza na kumuomba Mungu arejeze furaha ya wokovu na kumtumikia katika nafasi aliyonipa. So, imekua ni process ilikua tayari nimeanza, nilipoona title tu ya prayers nikajua Mungu ana jambo anataka kufanya katika maisha yangu. Nmashukuru amerejesha furaha na shauku niliyokuwa nayo mwanzo ya kumtafuta na kumtegemea katika kila jambo.
Amerejesha shauku yangu ya kuandika pia ambayo ilianza kupotea, hata tu kuandika notes za haya masomo bila kughaili kwangu ni ushuhuda mana nilikua nimeshafika pabaya. Katika yote nazidi kujifunza kuwa mtii na kufanya yale yanipasayo kufanya Kama mwana.
Baba nakushukuru kwakua hujawahi choka kunilea na kunionesha njia sahihi, kila ninapopitia changamoto hujachoka kunishauri na kuniombea. Mungu akujaze pale ulipopunguza na akuhuishe maradufu.
All Glory to God in the highest!!

ESTHER MWAIJANDE
Ubarikiwe sana baba yangu. Nakosa hata maneno ya kuongea, naishia kusema UTUKUFU KWA MUNGU. Daddy umetumika kuyabadilisha maisha yangu kwa kiwango kikubwa sana maana nilipokuwa nimefikia ilikuwa ni kiuangamia tu. MUNGU NINALITUKUZA JINA LAKO.

HILALIA PHILIPO
Mungu ni mwema nashukuru Mungu kwa kunitia nguvu. Kuna jambo ambalo nilitaman kulianza mda mrefu sana lakin sikuwa na hamasa ndani yangu kulifanya lakini baada ya kuanza maombi haya na kumuomba Mungu anirejeshe katika nafasi yangu katika suala zima la KUTUMIKA  nikajikuta ninapata nguvu ya ajabu na hamasa Moyoni mwangu kuanza upya na kuendeleza plans ya jambo nililokuwa nataka kufanya.
Na pia napenda kumshukuru Mungu naona mabadiliko katika suala zima la MAOMBI. Nimeona ni namna gani MUNGU kanitengenezea utulivu flan amaizing katika maombi na kuwa na shauku ya kuendelea kuomba.
Pia katika suala zima la kujifunza. Hili suala la NAFASI lilikuwa jambo jipya na limenifanya nikakumbuka WOKOVU niliokuwa nao wakati nauanza na kujigundua asilimia 200% nilikuwa nilishapotea na kutoka katika wokovu huo. Yaan hata nguvu niliyokuwa nayo ilikuwa hakuna hata chembe. Ilikuwa like am forcing myself. But now i see GOD  ANANITENGENEZA UNTIL NOW. YAAN HAPA NIMETEKEWA KABISAA NA NGUVU ZA BWANA WA MAJESHI.
Dady Mungu aendele KUKUMIMINIA MIBARAKA na Mungu akupe haja za moyo wako.
Nakupenda baba.

DESTEA KAGINE
Mungu akubariki na akuinue kwa viwango vya juu zaidi Pastor Raphael. Kwa hakika huduma yako ni njema sana. Binafsi nimemwona Mungu sana kupitia maombi haya.

ELIZABETH KING
Hahahahah…….nianze hv tu, kwasababu siunajua kila kitu ulichokiwa unatamani kukipata sikunyingi sasa umekipata eee, so lazima uwe unacheka, unajua nikisema Mungu wetu ni mzuri kila mara nasema nikiwa na cheka bafuraha isiyo kifani si kwaaajili yangu tu bali na kwaajili yenu, MUNGU WETU AMETUKUMBUKA WAPENDWA,
1. Namshukuru Mungu mno kwakunipa ufahamu, maarifa, hekima, nimerejea kwenye nafasi, unajua kuna neno linasema walio wa Mungu, Mungu anawajua.. Hapo nilitaka kusema Baba umjua mwana, na mwana umjua Baba, sasa hivi nikisema mimi ni mwana wa Mungu sisemi kwa mashaka tena naamini hivyo na Baba anajua hivyo kuwa mimi ni mwanae, so baada ya kupata huo ufahamu, sasa sigombanii tena nafasi kwa Baba, nilikuwa na shida ya pesa kiasi fulani na nikawaza nitapata wapi, nilipo lifikisha ilo swala kwa mama, mama angu anatabia ya kuniuliza ya kazi gani, lakini ilo swali jana sikusikia nilitaja kiasi na nikapewa na zaidi, nambariki Mungu juu ya hili.
2. Nilikuwa niko vizuri mno najirani yangu ghafla akaanza nipita bila salamu ananipandisha ananishusha, nikasema moyoni huyu mdogo kwangu nitamwonesha kama mimi ni zaidi yake, nikajitenga mbali nae sasa tunaanza maombi nikakumbushwa kupatana na mtu alie nikosea ikabidi niende kuongea naye, nimuulize kulikoni mpendwa basi akanieleza yote nilio mkosea hadi kufikia hatua hiyo, na yote alinihisi tu haikuwa kweli kasoro moja ndo lilikuwa kweli, tukaombana msamaha tukapatana sasa hivi mambo ni shwari.
3. Nashukuru pia kwa maombi haya kwasababu yamenipa majibu mengi saana ya maswali niliokuwa kuwa nayo mengi ya kiroho na kimwili niliokosaga majibu kwa muda mrefu, kupitia maombi haya nimepata majibu yake, namrudishia sifa na utukufu Mungu.
Asante pia Pastor Raphael, wewe ni mtumishi wa Mungu ulonisaidia mno upande wa kiroho, Mungu akubariki saana wewe na familia yako, na aendelee kukuzidishia mara dufu, atimimize kusudi la huduma hii, uendelee kufanyika baraka na kwa wengine wengi... simalizi jamani Mungu akubariki mno.


REBECCA AMOS
Shalom jaman,, kwa majina kamili Naitwa Rebeca, nimepata fursa ya kuwa humu kwa kipindi chote.... niliingia humu kwa sababu ya title ya tangazo reposition nmetamani sana kwa kipindi kirefu kuirudia nafasi yangu kimungu ila nilikuwa nakosa pa kuanzia ..... nlipoteza taste ya maombi..... yaani safar yangu was vuru vuru, watu wa Mungu nlikua na muda finyu lakini kila nkikumbuka kua nataka kurudi kwa position yangu ilinipa hamu na hatua maana nliona hii kama nafas ya pekee,, toka ijumaa sa ni kama nimelishwa pilipili yaan duh ni haielezek kwanza amani ya moyo nliyonayo pili naona kama nimeokoka jana serious nimepata zaidi ya nlichotarajia maana nimekua connected than ever before. Nina furaha na raha,, nlishasahau kuomba na kupewa mistari ya kusoma now nikiomba nkimaliza tu nakuwa directed wap soma na nkisoma ni kama napita mule mule. Nlishasahau kuomba kwa machoz jamani sa hivi ni kama mvua et ,, sauti ya Mungu ilikua ndo kama nimesuswa jamani within hii time ni kama rafiki ananisemesha sijui sa hata niseme nini, Dad nakupenda members nawapenda Mungu atuimarishe.

GRACE
Namshukuru Mungu kwa maombi na mafundisho kuna mambo ambayo nilikuwa nafanya kanisani nikaja nikaacha nilipokuwa naanza maombi nikajiona jinga sana  ila leo nimeanza kufanya na ninaamini nitaendelea kufanya na zaidi, Mungu akubariki dady tangu nimekufahamu sijajuta naamini Mungu atazidi kukutumia na zaidi tutafaidi matunda mema aloweka kwako u zaidi ya mwl zaidi  zaidi ya baba hakika, Mungu akutunze nimejifunza mengi kutoka kwako ubarikiwe wewe na familia yako kwa somo la Repositioning nimemwona Mungu yaani kiasi ambacho sijawahi kabisa.

LAWRENCIA MASHIKU
Baba asante hata sasa sipo kama nlivyokuwa ..nashukuru Mungu kwa ajili yako pastor Mungu akubariki...ushuhuda wangu bado upo jikon....ila najiona watofauti saaaana.

MARIAM MWANTOGA
Namshukuru sn Mungu nimemuona kwa namna nyingine kabisaaa.
Ni miaka kadhaa imepita tumekua hatuna ibada ya pamoja na familia yangu, Mungu kanirejesha kwenye nafasi niliyo ipoteza leo tumefanya ibada ya pamoja.
Mungu nakushukuru pokea sifa za Moyo wangu, uinuliwe Bwana, pokea utukufu ee Mfalme.
Dady Raphael Mungu akuhuishe na kukupa haja ya Moyo wako, akailinde familia yako kwaajili ya utukufu wake.


HOYCE FRANK
Nina mshukuru sana Mungu nimejifunza nakujua mengi san nakujijua mimi nani nilikuwa nashiriki sana mambo ya kanisa niliacha ile leo nimeenda na nitaendelea kwenda na nimejua nafasi yang na nimejijua mimi nani asante sana pastor.

JANE MZIRAY
Kupitia maombi Haya Mungu kanionyesha kitu cha ajabu Sana. 
Kuna mtu alihamia katika eneo ninalofanyia kazi na yeye akiwa mfanyakazi katika sector nyingine  na akataka niwe rafiki yake.  Sasa baada ya kuwa bad. Muda ukapta kuna mambo flan flan akawa anayafanya na nilvyomshtukia nikakosa amani nae kabisa na nikagundua vitu vingine ambavyo ni nje ya mapenzi ya Mungu... Sasa basi mimi nikamueleza tu ukweli kwamba kutokana na mambo aliyo nayo siwez kuendelea na urafiki uwe.... Kuanzia nilipomueleza hivyo nilibadilika sana nikawa mtu mwenye hasira za ajabu nagombana na watu hadi wenzangu ofisini.. Nikiambiwa kitu kidogo tu nakuwa mkali na mwenyewe hasira sana hadi nikawa najichukia mwenyewe..
Jana nilvyokuwa kwenye maombi Mungu kanionyesha  kumbe huyo ndo chanzo cha haya yote kwa hyo what I know niliingia kwenye maombi na kuikataa ile hali na kuomba maombi ya ukombozi... Bado ninahitaji Hekima Ya Mungu ili niweze sasa kutengeneza na wale ambao nimeshaharibu kwao. Kwa hiyo namshukuru sana Mungu kwa hilo jaman..

ESTHER WILLIAM
Kwa kweli namshukuru sana Mungu kupitia haya maombi, vilinyeyuka vita juu yangu,tangu ijumaa, kama ningesikiliza mahubiri ya kipepo kwakweli nisingevuka ningebaki kama nilivyo. Mungu ni mwema alinipa nguvu ya kutokutii vilivyo vikwazo vilivyojiinua,yaani ninaamani sana moyoni baada ya haya maombi sasaivi nasikia ule uamsho ndani yangu wa kuomba, ii hali ilikuwa imebalia ndani yangu neema tu ya Mungu, nilifikia hatua ya kuomba mi mwenyewe naona kabisa haya maombi sijui kama Mungu ameyasikia,yaani naona makavu. Ila sasaivi naomba huku naamini Mungu kayasikia, Mungu pokea sifa na heshima kwa kutukumbuka watishi wako tuliokuwa tumetolewa kwenye nafasi zetu, asante kwa kutulejesha Mfalme wa Amani tunakuinua Jehova.


QUEEN FLETCHER
Shalom famly,
Napenda kumshukuru sana huyu Mungu kwa ajili ya program nzima ya repositioning fasting.
Well safari yangu ilianza hapa kwa kusua sua lakini nimeimaliza kwa ushindi mkuu. Namshukuru Baba pia kwa mafunzo yote na miongozo.Mungu akutunze.
Ni maombi yangu kila mmja atayaishi na tuliyoyapanda na kuyaishi yote tuliyopata mahali hapa. Namshukuru sana Mungu kwa ajili Ya upya huu ninaoufeeel sasa. Tuombeane wapendwa. Target yetu kubwa n wote tukutane Mbinguni siku ile
Nawapenda .
Mungu awatunze wote.
Amen.


ESTHER MWAIJANDE
Wapendwa naomba na mimi niseme kitu, before closet prayers nilipoteza kiu ya maombi na kusoma Neno. Nilikuwa naomba kwa nguvu na kujikakamua sana lkn ukweli nilikuwa nilikuwa najua kabisa kwamba hapa hamna kitu. Kila nikishika biblia nasoma mistari miwili naacha, inaweza ikakata wiki sijashika kabisa bible. Nilikuwa najichukia sana but kuchukua hatua nilishindwa coz sikujua nianzie wapi.
Baada ya kuingia Closet Players tu siku ya kwanza moyo wangu ulipata amani na niliposoma notes za mafundisho nilihisi mlainisho flani kwenye moyo wangu. Namshukuru Mungu amenirudisha kwenye nafasi yangu, nikisoma Neno naelewa na kufunuliwa vitu kwa upana na kwa kasi ya ajabu, nikiingia kuomba naomba kwa wepesi sana.
Ninamshukuru Mungu sana kwa ajili ya ukombozi alioniletea kupitia mtumishi wake maana bila hivyo hali yangu kiroho ingezidi kuwa mbaya sana. Mungu anisaidie na kunipa hekima ya  kumantain hii nafasi. Mbarikiwe sana.
LORD I GLORIFY YOUR WONDERFUL NAME.


Hakuna maoni:

Inaendeshwa na Blogger.