Ads Top

NGUVU YA KUSIMAMA KATIKA NAFASI YAKO-1


NGUVU YA KUSIMAMA KATIKA NAFASI YAKO
By Pastor Raphel JL.

TUMEUMBWA KUISHI ndani ya NAFASI ZETU, kila mmoja.
Usahihi wa kila kitu tunachofanya umebebwa na NAFASI tunayoitumia kufanyia chochote kile.
Ninaamini kuwa moja kati ya sababu kwa nini maombi yetu hayajibiwi kwa wakati au hayajibiwi kabisa ni kuomba tukiwa NJE YA NAFASI ZETU.

NAFASI NI NINI?
Nafasi ni eneo ambalo mtu amepewa, au fursa au cheo ambapo mtu aliyepewa anatakiwa kufanya mambo yake yote au KUISHI MAISHA YAKE YOTE akiwa hapo. KILA ANACHOFANYA LAZIMA KIFANYIKE TOKEA KWENYE NAFASI YAKE.
NAFASI imebeba KILA KITU.
NAFASI imebeba HATMA.
NAFASI imebeba KIBALI.
NAFASI imebeba KANUNI.
NAFASI imebeba FURSA.
NAFASI imebeba WATU NA RASLIMALI zote unazohitaji kufanikiwa.
NAFASI imebeba UPENYO.
NAFASI imebeba MAFANIKIO YA KWELI.
NAFASI imebeba MAJIBU SAHIHI.
NAFASI imebeba SILAHA.

Mwanzo 3:9
Bwana Mungu akamwita Adamu, akamwambia, uko wapi?

Tunaona katika Mwanzo 3:9, Mungu anamuuliza Adamu, UKO WAPI-WHERE ARE YOU?
Hili ni swali la NAFASI-POSITION. Tungetegemea Adamu angeulizwa UMEFANYA NINI.....lakini hakuulizwa hivyo, kwa sababu, UNACHOFANYA KIMEFUNGWA KWENYE NAFASI......
Kwa lugha ingine, Mungu anajaribu kuonesha hapo kuwa Adamu angekuwa kwenye NAFASI YAKE asingekosea kwa kumkubali mkewe kula tunda alilokatazwa. Kumbuka ADAMU HAKUDANGANYWA NA NYOKA BALI EVA. Aliyedanganywa ni Eva, ndiye alianza kukosea lakini Mungu alipokuja hakuuliza EVA UKO WAPI kwani kila mtu ana nafasi yake. ADAMU NI KIONGOZI KATIKA UONGOZI, EVA NI KIONGOZI KATIKA USAIDIZI.
ADAM IS A LEADER IN A LEADING ROLE AND EVE IS A LEADER IN A HELPING ROLE. THEY ARE ALL LEADERS BUT IN DIFFERENT POSITIONS.
Eva asingekosea kama ANGESIMAMA na KURIDHIKA na NAFASI YAKE ya kuwa MSAIDIZI WA KUMFAA ADAM. Ila tunaona wote wawili walikosea. Eva alikosea kwa kuwa alitoka NJE YA NAFASI YAKE. Na Adamu alikosea pia kwa kutoka nje ya NAFASI YAKE....How?
Eva alipofuatwa na nyoka alitoka kwenye nafasi yake kwa UJUAJI WAKE.
Adamu alitoka kwenye nafasi yake na akala tunda kwa HURUMA ZA KIMAPENZI KWA MKEWE.
Eva angebaki kwenye NAFASI yake kama angemwambia nyoka, SIWEZI KUKUJIBU MPAKA KIONGOZI WANGU AWEPO.
Adam asingekosea kama ANGEMSIMAMIA VIZURI mkewe.

KILA MTU ALIKOSEA AKIWA NJE YA NAFASI, lakini Mungu alipokuja akamuuliza KIONGOZI-MUME....UKO WAPI....Mungu hakuuliza MKO WAPI?
DIVORCE nyingi zinatokea kwasababu kila mtu anakuwa NJE YA NAFASI yake.....
Wanawake wanataka kuishi na kuwa kama wanaume. Wanaume wanataka kuishi na kuwa kama wanawake.

MAHUSIANO MENGI YAMEKAA KISHINDANI.
NDOA NYINGI ZIMEKAA KISHINDANI KWANI KILA MTU ANATAKA KUFANYA AFANYALO NJE YA NAFASI ALIYOPEWA.
Kukaa na kuishi nje ya NAFASI ndio msingi wa uharibifu wa mambo mengi sana mpaka leo.
UKO WAPI? Hili ni swali gumu sana. Na ukisoma Biblia utaona watu hutoka kwenye nafasi zao kidogo kidogo. Lakini sababu kubwa ni pale mtu anapofika na KUMKATAA MUNGU KATIKA FAHAMU ZAKE. Yaani kutokukubali MAMLAKA ya Mungu ifanye kazi ndani yake. Kutaka uhuru usio na mipaka.

Warumi 1:24-27
Kwa aili ya hayo Mungu aliwaacha katika tama za mioyo yao, waufuate uchafu, hata wakavunjiana heshima miili yao. Kwa maana waliibadili kweli ya Mungu kuwa uongo, wakakisujudia kiumbe na kukiabudu badala ya Muumba anayehimidiwa milele. Amina.
Hivyo Mungu aliwaachia wafuate tama zao za aibu, hata wanawake wakabadili matumizi ya asili kwa matumizi yasiyo ya asili; wanaume nao vivyo hivyo waliyaacha matumizi ya mke, ya asili, wakawakiana tama, wanaume wakiyatenda yasiyopasa, wakapata nafsini mwao malipo ya upotevu wao yaliyo haki yao.

Unaona hapo WALIVUNJIANA HESHIMA MIILI YAO.....maana yake walianza kuitumia miili yao kinyume na namna iliyoumbwa na vile inavyotakiwa kutumika. KINYUME NA MAUMBILE. USHOGA NA USAGAJI.
Ukiwa kwenye mahusiano na kila kitu unataka kifanyike unavyotaka wewe ujue wewe  ni MSHINDANI na sio MKAMILISHAJI.....YOU ARE THERE TO COMPETE, NOT TO COMPLETE.
NAFASI IMEBEBA USHAWISHI.
Kukaa nje ya nafasi zetu, ndio kinatufanya hata tunapoomba tunaomba kama Mungu ni msela wetu mpaka wakati mwingine TUNAMFOKEA kabisa.
Mtoto anaejua nafasi yake kwa Baba yake, anapokuwa anaomba kitu huwa anakuwaje vile?
Kutokujua nafasi zetu kumetufanya sisi tulio watoto wa mfalme tuishi kama watumwa na watumwa wandunda tu kama watoto wa mfalme. ASANTE UJINGA.

Huwa tunatolewa nje ya nafasi zetu kwa NGUVU YA USHAWISHI inayochanganyika na kiwango fulani hivi cha ujinga.



ITAENDELEA......

Maoni 1 :

Inaendeshwa na Blogger.