Ads Top

NGUVU YA KUSIMAMA KATIKA NAFASI YAKO-2

BY PASTOR RAPHAEL LYELA

...INAENDELEA (soma sehemu ya kwanza)


Ndio maana utaona watu wengi, hata mahusiano mengi huwa yanaharibika zaidi kwa ushauri wa nje kutegemea ushauri huo unatoka wapi.
Mithali 1:10
Mwanangu, wenye dhambi wakikushawishi, wewe usikubali

Kwenye eneo la ndoa, kwa mfano.....kinafasi, A MAN IS A LEADER. A WOMAN IS A HELPER.....kila mtu mwenye kutaka kufurahia ndoa yake lazima aanzie hapo.....ni hatari kugombania nafasi ya mtu mwingine.....
NAFASI IMEBEBA WAJIBU.
Wewe jiulize kama Adamu angewajibika. Kama Eva angewajibika. Au kama wewe ungewajibika kwenye nafasi yako, mngepigana vibuti? Mngeachana?
NAFASI IMEBEBA UFAHAMU.

Mwanzo 3:9
Bwana Mungu akamwita Adamu, akamwambia, uko wapi?

Kuna mahali au kuna nafasi Mungu alimpa Adamu.....UKO WAPI.....ni kama Mungu anasema.....Adamu kuna nafasi nilikuweka mbona sikuoni?



Kuna watu wanakuja kwenye maisha yetu ili TUWASAIDIE waweze kupiga hatua, ila kwakuwa huwa hatujui nafasi zetu unakuta watu wanaishia kutongazana, kwa nini usipigwe kibuti? Mtu amekuja ili awe mwanafunzi na mfuasi wako katika Bwana, wewe unaanza kuleta stori za mapenzi......laiti kama tungejua.....ndo maana kuna watu unaweza hata usijue lini walipotea na kuondoka karibu yako....kumbe ulianza kuongea pumba nje ya nafsi yako......

Kuna nafasi aliyonipa Mungu kwenye mahusiano yangu na wewe.
Kuna nafasi natakiwa kumpa Mungu ndani yangu.
Kuna nafasi yangu kwa mke wangu.
Kuna nafasi yangu kwa watoto wangu.
Kuna nafasi yangu kazini.
Kuna nafasi yangu kanisani.
Muheshimu mtu ambaye unajua amekupa nafasi ambayo neon lako moja linaweza kuathiri maisha yake yote. JE MUNGU SI ZAIDI?

Mwanzo 3:9...
9 BWANA Mungu akamwita Adamu, akamwambia, Uko wapi?

Mungu alimuuliza Adam...UKO WAPI? Ingawaje aliyekosea na kusababisha kosa ni Eva lakini Mungu hakumuuliza Eva UKO WAPI.....tuendelee kidogo
NAFASI YA MUME KAMA KIONGOZI HAIWEZI KUCHUKULIWA NA UJUAJI WA MSAIDIZI WAKE,BADO ATAWAJIBIKA TU
Watu hutoka kwenye nafasi zao zao kidogokidogo kwa ushawishi ujinga.
Mwanzo 3:10 inasemaje?

Mwanzo 3:10
Akasema, Nalisikia sauti yako bustanini, nikaogopa kwa kuwa mimi ni uchi; nikajificha.

Utaona hapo kuwa mtu ukiwa kwenye nafasi isiyo yako kuna mambo yanatokea...kwanza kila utakachofanya utakosea hata kama kitawafaidisha wengine lakini pia HATA KUJIBU UTAKOSEA.
Adam aliulizwa UKO WAPI....akajibuje?
Ndo maana nimekuwa nasema kuanzia mwanzoni kuwa hata maombi yetu mengi tunaweza tukaona HAYAJIBIWI kumbe shida ni NAFASI tunayoiyumia kuomba hayo maombi.
Ni kama kusema maombi pekee ambayo Mungu ameonyesha kuyasikia nakuyakubali na mtu akiwa nje ya nafasi yake ni maombi ya TOBA,yaani maombi ya kugeuka.
Ukiona uko kwenye mahusiano na unaona kila siku ni magomvi,yawezekana kabisa kuwa huenda mko kama Adam na Eva...nje ya nafasi zenu...nje ya nafasi ni KUJILAUMU NA KULAUMIANA TUUU
Ni kweli kuwa Adam alimwambia Mungu kuwa ni huyo mwanamke aliempa...lakini je alikwepa LAANA?
Adamu aliulizwa UKO WAPI....akakosea kujibu kwani alikuwa nje ya nafasi yake....Eva aliuzwaje?
Mwanzo 3:13 tusome.....
13 BWANA Mungu akamwambia mwanamke, Nini hili ulilolifanya? Mwanamke akasema, Nyoka alinidanganya, nikala.

Utaona hapo kuwa Eva hakuulizwa UKO WAPI....aliulizwa UMEFANYA NINI kwani ile nafasi aliyofanyia alichokifanya haikuwa yake ndo maana alikosea na lakini haikumfanya akose LAANA na yeye. Kuitumie nafasi ya mwingine kukosea hakukufanyi wewe uwe salama.
So mke anapotoka kwenye nafasi yake na kuanza kudai haki yake,ataishia kupigwa tu na mwisho hata ndoa inaweza kuvunjwa...

Mume naye hivohivo akitoka kwenye nafasi yake ya uongozi na kuanza kufanya anayofanya ataishia kuleta ubabe tuuuu



ITAENDELEA....

Maoni 1 :

Inaendeshwa na Blogger.