Ads Top

NGUVU YA KUSIMAMA KATIKA NAFASI YAKO-4



...INAENDELEA

UTAJUAJE KUWA UKO NJE YA NAFASI
DALILI ZA MTU ALIYE NJE YA NAFASI YAKE

WARUMI 11:29
[29]Kwa sababu karama za Mungu hazina majuto, wala mwito wake.

Yakobo 1:17
[17]Kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu, hushuka kwa Baba wa mianga; kwake hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeuka-geuka.

UKIONA HUNA AMANI IPITAYO FAHAMU ZOTE-ujue umetoka kwenye nafasi yako
UKIONA MAJUTO NA KUJIHUKUMU-Ujue umetoka
UKIONA HUNA FURAHA YA BWANA-Ujue umetoka
UKIONA PIA KUWA UMEANZA KUPOTEZA SHAUKU NA HAMU YA KUFANYA JAMBO,huenda ikawa kabisaa kuwa umetoka
Ukiona umejaa huzuni na malalamiko na masikitiko
Ukiona HUPATI UTOSHELEVU
UKIONA ULICHOKUWA UNAFANYA ZAMANI NI HERI KULIKO UNACHOFANYA SASA-huenda umetoka
Ukiona umejaa kujitetea au kujiheabia sana haki...huenda umetoka
Kumbuka KARAMA AU ZAWADI toka kwa Mungu HAZINA MAJUTO
Ukitoka kwenye nafasi yako HATA MACHO YAKO YAANZA KUONA VIBAYA
Ukitoka kwenye nafasi yako UZURI HUGEUKA UBAYA kwa haraka sana

Watu wameacha kazi kisa, mishahara haitoshi...wakaenda kwenye mishahara mikubwa na kumuacha Mungu kwenye mshahara mdogo-wanahangaika kama wafungwa na watumwa

Watu wameacha kazi vijijini ili wawe mijini,wamemuacha mungu kijijini na wako mijini wanahenya-kumbe mjini ni mungu pia...hatari sana
Ishu sio mshahara mdogo...issue ni uko kwenye nafasi? Hakuna siku wafanyakazi wote duniani watalipwa mishahara inayofanana. Au wote wakafanya kazi vijijini...ila unapotaka kuhama au kubadilisha kazi, je umeomba ruhusa? Umeruhusiwa?
Uliomba kupata kazi ukapata. Mbona unajiondokea?
Watu wanafukuzia pesa, vyeo, kukaa mijini...wako tayari kufanya hayo yote hata bila mungu...watu wanapenda kuteseka. Wengi wanafurahia.

Ukiwa kwenye nafasi isiyo yako hata uelewa wako unabadilika
Tulia bana
Nilijifunza kutulia
Nilipoanza kazi nilikuwa na take home ya 470,000...niliona watu wakiacha kazi na kwenda kwenye Malipo makubwa...MWISHO niliwaona wakirudi tena
Magomvi mengi sana kwenye ndoa na mahusiano yangeisha kama kila mtu angesimama kwenye nafasi yake
Mwanaume akikaa nafasi ya mwanamke anageuka kuwa kama dudu
Mwanamke akikaa kwenye nafasi anageuka kuwa kama mganga wa jadi
Nimeona watu wahama mikoa, kisa hawaipendi....wanaenda kwenye mikoa inayoonekana mizuri kama kule alikoelekea Loti ambako ndo Sodoma ilikuwepo....Wanaacha mikoa ambayo wao hawaipendi....wanamuacha na Mungu huko...wanaenda mikoa mizuri bila Mungu
Nimeona vijana waliosoma kozi ambazo haziko kwenye nafasi zao chuoni...wanaishi maisha ya kuchukia kazi zao maana hawakupenda tokea mwanzo ila waliambia KOZI HIYO INA MKOPO....mwanasheria anaishia kuwa BANK TELLER
Unaweza kupewa kazi inayoweza kukusaidia kukutoa kwenye nafasi yako....be very careful sana....
Kuna watu utendaji kazi wao unadolora toka walivyopewa promotion...promotion sio mbaya ila ikija nje ya majira inaweza kuwa ishara kwamba unaenda kufukuzwa kazi hivi karibuni
Kuna viongozi wanapobadilishiwa tu nafsi zao huanza kufanya vibaya kama vichaa

Kwanza IJUE NAFASI YAKO...
Pili USHIRIKA NA ROHO MTAKATIFU...LAZIMA UTAJUA TUUU




Wengine wamechelewa kuoa na kuolewa kwani waliwaacha waume na wake zao kwenye maeneo ambayo hawakuona kama mtu mzuri na sahihi anaweza kutokea huko...hata uende kwa the greatest apostel of all time hakuna maombi ya kukupa mtu sahihi labda maombi ya kulazimishia ambayo yatakugharimu milele....unakaa unajiona kama una mkosi kumbe umejikosisha mwenyewe.
Ushirika na Roho Mtakatifu ndio ufunguo wa kweli.
Kutokujua nafasi yako kunaweza kukufanya ukubali hata offer za uharibifu.
Ni rahisi sana kuoa na kuolewa na jiwe au nyoka kama uko nje ya nafasi yako.

Nje ya nafasi yako utawasingizia watu hata kwa makosa yako mwenyewe
Kama huijui nafasi yako, usiombe kurudishwa kwenye nafasi na huijui.
JE, WAIJUA NAFASI YAKO?
KAMA HUIJUI BASI IJUE
JE,UMETOKA KWENYE NAFASI YAKO? BASI RUDI...sema tu kurudi lazima kuna gharama
MUNGU AKUSIMAMISHE.

Ukijua NAFASI YAKO,HUNA HAJA YA KUSHINDANA

ITAENDELEA...

Hakuna maoni:

Inaendeshwa na Blogger.