Ads Top

NGUVU YA KUSIMAMA KATIKA NAFASI YAKO-5





...INAENDELEA

Ukijua nafasi yako unapata utulivu fulani wa ajabu ambao unakwambia Mungu ndio utoshelevu wako.
In your position, no competition.

Mtoto asiyejua NAFASI yake kwa baba yake  hana tofauti na mtumwa. Ni heri mtumwa
Mhubiri 10:7-HIKI NDO KIWANGO CHA JUU KABISA CHA KUKAA NJE YA NAFASI,UTAKUWA KAMA OMBAOMBA NA HUKU BABA YAKO ANAMILIKI VYOTE.

Mhubiri 10:7
7 Mimi nimeona watumwa wamepanda farasi, na wakuu wakienda kwa miguu juu ya nchi kama watumwa.

Ona Mhubiri 10:6
6 ya kuwa upumbavu huwekwa mahali pa juu sana, nao wakwasi hukaa mahali pa chini.
Mungu akupe hatua

Akuhamishe mahali ulipo
Akupeleke unapostahili,sio tu unapotaka
Ukigundua umetoka nje ya NAFASI fanya TOBA NA KUOMBA REHEMA.
Jifunze utofauti wa TOBA NA REHEMA.
Wengine mmezifanya familia zenu kuwa masikini na ombaomba kisa hamtaki kusimama  ktk nafasi zenu
SIMAMA MAHALI PALIPOBOMOKA
Maombi mepesi na rahisi kujibiwa na Mungu ni TOBA NA REHEMA.
Sijasema usiache kazi au usihame...MBINGU ZIMEKUBALI?? UMERUHUSIWA??
Stay in your position
Stand in your position
If you are a woman, your position is not the assistant but a helper. Assistants can overflow their bosses, not you.
Kudai haki nje ya nafasi yako ni kujiumiza
Haki sawa kwa wote wakati wanaodai wenyewe hawako sawa?
Huwezi kuijua haki yako kama uko nje nafasi yako
Kusimama imara kwenye nafasi isiyo yako ni kujivuruga.
Usikubali kuoa na hujui nafasi yako
Unakubalije kuolewa na hujui nafasi yako?
Mtaenda kuanza kugombania nafasi mpaka mmemalizana
Kaa kwenye nafasi yako bana
Usipojua nafasi yako kwa mtu utaishi kwa kujistukia sanaaaaa

Bwana Yesu akawaambia wanafunzi wake....SIWAITI TENA WATUMWA...au kwa lugha ingine NAWAHAMISHA NAFASI YENU..FROM WATUMWA TO FRIENDS...ukihamishwa nafasi hata marupurupu yanahama na kuongezea au kupungua pia
MUNGU AKUFUNGUE MACHO
Watu wengi sana tuna alama ya KOSA LA LUTU/LOTI
Ukiwa kwenye nafasi isiyo sahihi ni rahisi sana kukutana na watu wasio sahihi
Ukiwa kwenye nafasi isiyo sahihi ni rahisi sana kuwa kwenye eneo lisilo sahihi

Wrong position-wrong people-wrong places
Lutu alitumia macho yake ya mwilini kuamua upande upi wa kwenda
Lutu aliongozwa na mazingira kama wenzangu na mimi ambao huwa wanaongozwa na mazingira, wakipangiwa kazi vijijini wanaona kama watachelewa kuendelea...NI HERI UPANGIWE KIJIJINI NA MUNGU PAMOJA NAWE kuliko kujipangia mjini bila Mungu.
Nakumbuka nilipokuwa nahamia Dodoma, tokea Arusha khaaaaaaaaaa nilionekana kama mpinga Kristo...back in 2011...watu wanaingalia Dodoma wanaona kama nini sijui...lakini nikagundua shida kubwa ni vile watu HULINGANISHA...waliiangalia Dodoma kwa macho ya Arusha...hivo sivyo watu wa Mungu wanavyoangalia mambo.
Hatuendi kwa kuona au kusikia.
Tunaenenda kwa imani-hakika ya mambo ninayotarajia-bayana ya yale ambayo bado sijayaona kwa macho
Macho haya yanakosesha sana kwenye maeneo mengi sana...
EDEN-Hili lilikuwa eneo sahihi kwa Adam na Eva. Eneo sahihi, nafasi sahihi.
Walipotoka tu kwenye nafasi yao, wakaondolewa hata eneo-location.
Kuna watu wanaishi kwa kutangatanga sanaaaaaaaa
Hawatuliii, watu wanahisi WAMELAANIWA....
Wanaenda kuombewa na MANABII NA MITUME waliopotoka ili kuvunja LAANA .na kumbe kumbe mtu kajilaani mweyewe kwa kuwa yuko NJE YA NAFASI....
Anaombewa weeeeeeeeeeeee, miaka nenda rudi… KUOMBEWA NA UKO KWENYE NAFASI ISIYO YAKO NI KUMFAIDISHA ANAEKUOMBEA maana wewe unakuwa huna akili zako tena....
Kabala ya kuombewa upate mume sahihi ni lazima uwe kwenye nafasi sahihi...yaani uwe na ufahamu sahihi wa wewe ni nani mbele za Mungu.
Kabla hujaenda kuombewa kwenye jambo lolote,jiulize...niko kwenye nafasi yangu....ama sivyo toba na rehema inakuhusu sana.

Kiwango cha kukosea ukiwa ndani ya nafasi yako hakifanani na kama ukiwa nje ya nafasi yako.

ITAENDELEA...

Hakuna maoni:

Inaendeshwa na Blogger.