Ads Top

SHIRIKI



SOMO: SHIRIKI
By Raphael JL

Niseme hivi....
Hii nukuu hapa....
Quotes by Raphael JL:Shiriki mambo ya watu na watu watashiriki mambo yako. Kuwa sehemu ya timu au kundi halafu hufanyi mambo yaliyomo ni sawa na kutengeneza mazingira ya kuwalaumu wengine kwa ubora wa ujinga wako. TRANSFORMATION IS ENGAGEMENT.
Mungu Kwanza-YKM!

Nataka niseme kuhusu jambo hilo maana linanipigisha kwata moyoni
Kwanza naamini Transformation is a function of TOTAL ENGAGEMENT....

Niwahamasishe wapendwa watu wakuu
MAISHA NI WATU. MAISHA NI MUNGU. Ukiwa na WATU WENYE MUNGU wanakuzunguka ujue umeshinda sana. KUSHIRIKI ni zaidi ya KUWEPO. Kushiriki ni zaidi ya kutoa fedha. Kushiriki ni hata kutoa taarifa unayodhani inawafaa wengine.
Hivi ninyi hamjaona kuwa kuna matukio ya maisha ya baadhi ya watu HUCHUKULIWA KWA NGUVU ZAIDI kuliko wengine? Hamjaona? Na wengi bado hamjaoa, Hamjaolewa, mtaihitaji watu kwenye maisha yenu itakapofikia matukio hayo.
Najua mna watu wengi maana mko kwenye magroup zaidi ya 666. So inawezekana group la YKM lisiwe na nguvu na thamani saaana...ila inaleta gap moja kubwa sana...
Kuna watu toka uchumba wao watu wameshiriki mpaka ndoa, Kuna watu inasikika juu kwa juu tu, Na wote wako humu humu. Kuna watu wanafiwa kimya kimya. Kuna watu hata akiumwa mafua tunajua
YOU CAN’T BE TRANSFORMED WITHOUT ENGAGEMENT...

Kuna watu hawajaona umuhimu wa kukutana pamoja physically. So hawamaanishi sana hata mkikubaliana kukutana hawajali sana. Ila kesho na keshokutwa watalalamika kuwa NO BODY CARES...bila kujua kuwa inaanzia kwao.
NI KWELI MUNGU ANAANGALIA MOYO, ILA SISI NI WATU, SO TUNAANGALIA MWILI.
Kama upo kwa group au timu na umekubali kuwepo kwa hiari yako... KUTOSHIRIKI MAKUBALIANO YA TIMU ni UASI.
Ukiwa na mchumba asiefanya mnayokubaliana? Ukiwa na mpenzi anaekutia moyo kwa maneno na sio matendo? Jikague kuanzie kwenye FAMILIA YAKO. Nenda kazini kwako. Nenda kanisani kwako. Utaona hii kanuni...WATU WANAOKUMBUKWA POPOTE WALIFANYA KITU...walishiriki
Moja kati ya kanuni ya THE VALUE OF YOUR IDENTITY tulijifunza camp inasema hivi..... YOUR PHYSICAL PRESENCE HAS NO SUBSTITUTE.....
Mara nyingi huwa nakuja humu na kusema hili na lile...because I know my presence matters

"YKM Dar ndo group ambalo nakuja mara nyingi zaidi kuliko any other group...ni kwasababu MKO ACTIVE sana.....na mna ushirikiano ila bado kuna watu wa kuwasaidia pia...walio kimya"
Haijulikani bado wako au hawako kitambo. Haijulikani wanaamni tunachokifanya au hawaamini. HAIJULIKANI tuuuu. Kuna wengine wakiombwa kuwa viongozi wanakataa...haha hahahah
SASA UTAJUAJE BILA KUFANYA? UTAFANYAJE BILA KUANZA? UTAANZAJE BILA KUWEPO NA CHA KUFANYA?
Najua humu wamo watu tofauti tofauti...wakubwa kwa wadogo...waliooa na kuolewa na ambao bado...so kila kundi linatakiwa lijue namna ya kumchukulia mwingine
Maana hata mimi mwenyewe nikisema nijihesabie haki kwa STATUS QUO ni vigumu kuwepo humu na kupiga story na watu tunaofanana tu kuvuta oxygen labda....So wakati mwingine wale waliooa na kuolewa...yaani toka walivyooolewa au kuoa hahaha haha ndo ikawa mwisho...khaaaaa MUNGU ANWAONA.
Kuna watu wamo humu hawana ajira...ila kuna watu wamo humu wana maconnection na wenye ajira...ila sema ndo vile sasa...NO ENGAGEMENT....
Kuna watu hawajaona umuhimu wa kuja camp...kuna watu hawawezi kukosa camp...kuna watu wanatamani kuja camp...wote wamo humu...camp haijalishi umeoa au umeolewa...in fact UKISHIKILIA STATUS QUO camp inaweza kukusumbua sana maana utaona aaah mambo ya vijana hayo...ila ukija unagundua khaaaaa mweeee
Katika kufuatilia jambo hili nikagundua pia ipo ishu ya KIPAUMBELE/PRIORITY...like YKM ni kipaumbele cha ngapi katika huduma ulizonazo au katika makundi ulonayo...HILI NI JAMBO BINAFSI...
Basi watu wa Mungu,nikajisemea tu kuwa niwatie moyo kwa tumaneno hutu tuchache...
SHIRIKI. ENGAGE.
Sio kila siku wewe utapokea tu. Kuna siku unaamua kutoa hata kama ni kwa kujitoa ufahamu.
WENEED EACH OTHER.
USHIRIKI UNALETA UMILIKI.
Ndo maana kila mtu akitokaga camp anakuwaga na moto mbaya...wengine moto huzimika baada ya wiki moja na wengine mpaka leo wamesimama.Lazima kuwe na siri. SHIRIKI. Kumbuka kushiriki kuna gharama yake. Ukiikimbia gharama ujue umekimbia kuwa matokeo ya mchakato wake.
NI HAYO TU.
MUNGU AWABARIKI
YKM
FICHUKA
MUNGU KWANZA

JESUS UP

Hakuna maoni:

Inaendeshwa na Blogger.