Ads Top

MOVE WITH MOVERS CAMP : MAMBO YATAKAYOTUSAIDIA KUTEMBEA NA MUNGU NA Mwl. MGISA MTEBE.





Amosi 3:3
Kupatana ina maana zaidi ya kukubaliana bali ina maana pia ya kuwa na Roho Moja pamoja na mwendo unaofanana. Hivyo lazima tupatane katika Roho moja na mwendo mmoja na Mungu ili tuondoke naye.

Kama Roho wa Mungu anapokoa anaondoka[MOVE] huo ndio unapaswa kuwa mwondoko wetu pamoja na ROHO WA MUNGU.
Wagalatia 5:25

“Kiwango cha ushindi na mfanikio katika kile ambacho Mungu amemuita mtu kufanya kinategemea sana ufahamu na ujuzi [Knowledge and Understaing] wa NAMNA Mungu anavyofanya kazi”

Mungu ana namna yake ya kufanya kazi. Usijifunze namna Mungu anavyofanya kazi kazini bali jifunze kabla ya kazi. Tunajifunza kuogelea kabla ya kuanza kuogelea. Tunajifunza kuzima moto kabla ya moto unaopaswa kuzimwa kutokea.

Mfano wa Daudi:
Aliandaliwa kwa Vita na kwa wito wake kabla hajaingia rasmi(full time) kwenye Wito wake.

Nidhamu ya Mfalme Daudi wakati wa Vita
Wito wa Daudi
1.    Kuwaunganisha Israeli
2.    Kupiga maadui wa Israeli; Alikuwa mtu wa vita sana
3.    Kuandika Zaburi

Wito wa Daudi ulikuwa katika perfect will of God lakini wito wa Sauli ulikuwa permitted will of God.

Sauli alipakwa mafuta kwa Kikombe[Man made] wakati wafalme na manabii wengine wote walipakwa mafuta kwa Pembe[God made]. Hapa ndipo maana kamili ya Perfect Will of God na Permitted Will of God. Yote ni Mapenzi ya Mungu.

Huwezi kuficha asili yako kama. Kama umejipa wito bado utafahamika tu kwa asili ya wito wako. Hadithi ya wazazi waliokuwa na mtoto wakilima shamba. Mara Fisi akelekea pale mtoto alipokuwepo walipokwenda wakakuta watoto wawili, baadae punda akaelekea pale na wakawa watoto watatu. Waliwachukua watoto wote bila kujua wa kwao ni yupi lakini katika Maadhimisho ya Siku ya kuzaliwa kwa mtoto wao waliweza kumtambua mtoto wao kwani mtoto mmoja alionekana migombani na mwingine kwenye mifupa lakini mtoto wao alibaki meza kuu kusherehekea.

Ushindi wa vita ya Daudi na Wafilisti ulitegemea UMAKINI wa
1.    Kuwa mahali sahihi; Kuwa na uwezo wa kutambua pale Mungu anapotaka kubadilisha mahali talipopaswa kuwa
2.    Kuwa na watu sahihi. Unatembea na nani?
3.    Kufanya kwa wakati sahihi
4.    Kufanya kazi kwa kasi







Katika Wito ulionao lazima ujue watu unaopaswa kutumika nao na uwaweke katika madaraja.

Watu walio chini yako lazima wawe na roho yako. Lazima wawe na wito kama ulio nao. Huduma isiwe ndani ya huduma nyingine.





Kukua katika WITO.
“If you miss the right level you listen wrongly”
            Ukiokosa nafasi sahihi utasikia vibaya.

Kiroho tunaongezeka ngazi kwa kushuka chini.

NAMNA YA KUTHIBITISHA WITO WAKO
Ishara au viashiria vya wito wa MTU
1.    Amani na Furaha ya moyoni(Peace and joy):
Mithali 10:22, Isaya 55:12, Filipi 4:4-7, Kolosai 3:15
Haiwekazekani Mungu akupe kitu ambacho kinakukosesha amani.
2.    Kupenda na kuridhika(Passion) kufanya jambo/kitu Fulani.
Passion ni msukumo wa ndani wa kupenda kufanya unachofanya hata kama haulipwi. Unaweza kudiriki hata kulipa ili upate nafasi ya kufanya hicho unachotaka kukifanya.
Kutoka 33:12-14, Mathayo 17:1-7, Zaburi 37:4, Zaburi 16:11
3.    Kutoa muda wa zaidi na ziada.
Kutoka 33:7-11, Mathayo 14:22-23, Marko 1:35, Yohana 8:1
4.    Uwezo mkubwa wa kazi hiyo(Ability)
Kutoka 31:1-5, Matendo 6:7-10
5.    Matokeo mazuri ya unachokifanya.
Yohana 5:31-36, Mathayo 11:3-5, Marko 16:15-20
6.    Wito Mungu inatajirisha[Baraka na Mafanikio]
Zaburi 1:1-3, Mithali 10:22, Mithali 17:8, Mithali 18:16, Kumbukumbu 8:12-18, 28:47-48
Mungu anafungua milango ya rasilimali fedha (utajiri) ili tumtumikie kwa furaha

Wito wa Mungu kwa mtu akitumika kwa uaminifu unalipa zaidi. Tunaweza kureplace taaluma sio wito
7.    Ushuhuda mzuri wa watu wengine. Watu wengine watakwambia. Na hii ni kutokana na matokeo ya kazi.
Mathayo 18:16, Yohana 6:11-14. Yohana 3:1-2, Matendo 6:1-8

Hakuna maoni:

Inaendeshwa na Blogger.