Ads Top

MOVE WITH MOVERS YOUTH CAMP : GROWING IN THE KNOWLEDGE OF GOD THROUGH CHRIST na APOSTLE SHEMEJI MELAYEKI




KWANINI KUMJUA MUNGU KATIKA KRISTO
Waefeso 1:17 “Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa utukufu awape ninyi roho ya hekima na ufunuo katika kumjua yeye

KUMJUA MUNGU kunahitaji Hekima na Ufunuo wa kumjua. Kama kuna kufunua kuna maficho yanayoficha ufahamu kumhusu Mungu

Mungu anafanuliwa kwa sababu amefichwa. Kuna namna watu hawamwelewi Mungu. Na kama humjui Mungu huwezi kuwa na uhusiano naye.

2 Petro 1:2 “Neema na iwe kwenu na Amani iongezwe katika kumjua Mungu na Yesu Bwana wetu
Neema na Amani inaongezwa kwa kadiri unavyopata ufahamu wa kumjua Mungu. Unapomjua Mungu unafahamu Mungu anawazaje, anatendaje,n.k

Epignosis[Greek word]Ă RecognitionĂ Full discernment, acknowledgement;
            This means the Highest Knowledge about somethings and not only just knowing.

2Petro 3:18 “Lakini kuweni katika Neema, na katika kumjua Bwana wetu na Mwokozi Yesu Kristo

2 Peter 1:3 “Kwa kuwa uweza awake wa Uungu umetukirimia vitu vyote vipasavyo uzima na utauwa, kwa KUMJUA yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe”

Kukirimiwa ni Kupewa kitu bila gharama yoyote (Zawadi)

MWILI NA DAMU (UFUNUO)
Mathayo 16:13-20
“Basi Yesu akaenda pande za Kaisaria-Filipi, akawauliza wanafunzi wake wakasema, Watu hunena Mwana wa Adamu kuwa ni nani? Wakasema, wengine hunena u Yohana Mbatizaji, wengine Eliya, Wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii. Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa nani. Simoni Petro akajibu akasema Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai. Yesu akajibu akamwambia Heri wewe Simoni Bar-yona; Kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni. Na ninakwambia, wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda”

Haiwezekani sana kupata ufunuo wa Mungu bila kuwa na Roho wa Mungu

Juu ya MWAMBA huu inamaanisha JUU YA UFUNUO huu;

Aina za ufunuo kuhusu Mungu
1.    Ufunuo wa roho
2.    Ufunuo wa Mwili na Damu

Mtu anaweza kuwa na ufunuo wa Mungu katika roho na Ufunuo wa Mungu katika Mwili na Damu. Ufunuo wenye uhakika kabisa juu ya Mungu ni ule utokanao na Roho wa Mungu.

Namna tunavyomjua Mungu inaathiri kila kitu katika maisha yako, kihuduma, kielimu, kiuchumi, n.k

KUHUSU KUMJUA MUNGU
1.    Watu wengi sana wanafikiri Kumjua Mungu Ni
a.    Kuwa na mistari mingi ya Biblia kichwani
b.    Jinsi unavyokuwa na nidhamu nzuri katika matendo ya Ukristo kama kuomba na kutoa Sadaka
c.    Kuepukana na ubaya na watu wabaya
2.    Sehemu kubwa ya uelewa wetu juu ya MUNGU HAUJAJENGWA KATIKA KWELI ILIYO KATIKA KRISTO YESU, BALI…
a.    Filamu za Kikristo
b.    Shuhuda za uongo makanisani kwa mfano Watu waliotoka kuzimu, watu wenye mapepo, shuhuda zilizokuzwa.
Kitu chochote ambacho kinapewa sauti kubwa kuwa mwangalifu nacho
c.    Mafundisho ya Hofu
Mungu ni mtakatifu sana kiasi kwamba anaweza kutakasa
d.    Mafundisho ya watu wenye nia Mbaya.

MJUE SANA MUNGU
Ayubu 22:21 “Mjue sana Mungu, ili uwe na Amani; ndivyo mema yatakavyokujia”
a.    Mstari huu ni maarufu sio kwa sababu ya watu kutaka kumjua Mungu lakini kutokana na mambo binafsi yanayotakiwa.
b.    Hii ni lawama na dongo analopewa Ayubu kutoka kwa Elifazi
c.    Watu wanasukumwa na selfish desire to get peace and prosperity and not KNOWING GOD

AYUBU ALIAMINI MUNGU NDIYE ANAYEMTAABISHA, Hii inaonesha kabisa kuwa hata Ayubu hakuwa anamjua Mungu vizuri.
Ayubu 23:16-17
“Kwani Mungu ameufanya moyo wangu kuzimia, Naye mwenyezi amenitaabisha

Mtazamo wa watu wengi wa zamani haukuwa katika kumjua Mungu kiuhalisia, ndiyo maana sehemu nyingi mabaya na mema yote walijua kuwa ni Mungu amewapatia

Ayubu 19:6-11
“Jueni basi kuwa Mungu amenipotosha, Na kunizingira kwa wavu wake. Tazama nalia, udhalimu, lakini sisikiwi, Naulilia msaada, wala hapana hukumu. Yeye ameiziba njia yangu nisipate kupita, Na kutia giza katika mapito yangu. Amenivua utukufu wangu, Na kuiondoa taji kichwani  mwangu. Ameiobomoa pande zote, name nimetoweka; na Tumaini langu ameling’oa kama mti

Ayubu 1:12 “Bwana akamwambia Shetani, Tazama, yote aliyo nayo yamo katika uwezo wako; lakini usinyooshe mkono wako juu yake yeye mwenyewe, Basi Shetani akatoka mbele za uso wa Bwana”

Hakuna mtu anayejua kutenda haki kwa kutenda vizuri.

Kabla ya Yesu kuja hatukuwa na ufahamu kamili kuhusu Mungu, hivyo lolote ambalo lilifanyika duniani liwe zuri au baya lilisababishwa na Mungu.

Ayubu 38:1-2
“Ndipo Bwana akamjibu Ayubu katika upepo wa kisulisuli na kusema, Ni nani huyu atiaye mashauri giza kwa maneno yasiyo na maarifa.”

Ayubu 40:8 “Je, hata hukumu yangu utaibatilisha? Utanitia mimi hatiani, upate kuhesabiwa haki

Ayubu 42:3-6
“Ni nani huyu afichaye mashauri bila maarifa? Kwa maana nimesema maneno nisiyoyafahamu. Mambo ya ajabu ya kunishinda mimi, nisiyoyajua. Sikiliza, nakusihi, name nitanena; nitakuuliza neno, nawe niambie. Nilikuwa nasikiliza habari zako kwa kusikia kwa  masikio; Bali sasa jicho langu linakuona. Kwa sababu hiyo najichukia nafsi yangu, na kutubu katika mavumbi na majivu

Yesu alitufundisha maana ya kutubu katika hali ambayo si ya maombi.

KUTUBU ni kugundua na kubadilika katika maisha ambayo tumekuwa tukiishi

Kuna tofauti ya kuishi na kuomba toba. Toba sio jambo la kuomba, toba ni jambo la kuishi.

Metamoya ni Neno la Kigriki lenye maana ya kutubu lenye maneno mawili Metamorphosis 

AYUBU NI SAMPLE TU YA WATU AMBAO WALIFIKIRI WANAMJUA MUNGU LAKINI HAWAMKUJUA MUNGU
Huwezi kutumia 100% ya mawazo ya watu walioishi kabla ya Yesu kama njia ya kujenga ufahamu bora juu ya Mungu utakaokupa kumjua Mungu kwa namna ambayo utahusiana naye sawa sawa.

LAKINI KUNA NAMNA ILIYO BORA:

LOOKING FOR A MODEL OF GOD?
Matendo 17:22-32
Paulo akasimama katika Aeropago, akasema Enyi watu wa Anthene, katika mambo yote naona ya kuwa ninyi ni watu wa kutafakari sana mambo ya dini. Kwa sababu nilipokuwa nikipita huko na huko na kuyaona mambo ya ibada yenu, naliona madhabahu iliyoandikwa maneno haya, KWA MUNGU ASIYEJULIKANA. Basi mimi nawahubirini habari zake yeye ambaye ninyi mnamwabudu bila kumjua. Mungu aliyeufanya ulimwengu na vitu vyote vilivyomo, yeye kwa kuwa ni BWANA wa mbingu nan chi hakai katika hekalu…”

GROWING IN THE KNOWLEDGE OF GOD
Kama humjui Yesu huwezi kumjua Mungu.  Tunaweza kumjua Mungu bila kupapasa kama wengine walivyokuwa wanafanya watu wa zamani kwa Kumjua Kristo.

Waebrania 1:1-4
“Mungu, ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi Mwisho wa siku hizi amesema na sisi katika Mwana aliyemweka kuwa mrithi wa yote, tena kwa yeye aliufanya ulimwengu.Yeye kuwa ni mng’ao wa utukufu wake na chapa ya nafsi yake, akivichukua vyote kwa amri ya uwezo wake, akiisha kufanya utakaso wa dhambi, aliketi mkono wa kuume wa ukuu huko juu...

Mwisho wa siku hizi Mungu anasema nasi katika mwana sio kupitia Mwana. Hii ina maana kuwa Yesu akizizungumza ni Mungu amezungumza.

Siku za mwisho ina maana ya Siku ambazo Mungu hana mjumbe mwingine tena atakayekuja zaidi ya Yesu. Alipomleta Yesu alifunga ukurasa. Hatusubiri ishara nyingine ambayo Mungu ataileta bali Yesu ndiye mfunga na mfungua ukurasa wa siku za mwisho. Agano la mwisho limefungwa. Siku za mwisho zilianza baada ya Yesu Kristo kufufuka.

“God is in control enough not to do anything.God is in control in his job description”. Watu wengi wana nguvu lakini hawwana uwezo wa kujicontrol.

Kinachomsumbua Mungu ni Upendo wake sio uwezo wake. Uwezo wake humfanya kuwa na nidhamu ya kutokufanya chochote kibaya kwetu. Ukiweza kitu sio ufanye kila kitu,

YESU ALITUMIA MUDA MWINGI SANA KUREKEBISHA MTAZAMO WAO JUU YA MUNGU
Yesu alikuwa anaonesha upande sahihi wa Mungu

Kumjua Yesu ni kumjua Mungu asilimia 100%

Hakuna maoni:

Inaendeshwa na Blogger.