Ads Top

NGUVU YA KUSIMAMA KATIKA NAFASI YAKO-3



...INAENDELEA

ZIPO DALILI ZA KUONYESHA KAMA UMETOKA KWENYE NAFASI YAKO

Ila kabla sijazisema hizo dalili, niseme hivi ukishaijua nafasi yako unahitaji nidhamu kuitunza na kuitumikia hiyo nafasi. Unahitaji ufahamu sana kuitumikia hiyo nafasi na unahitaji HEKIMA.
Mfano: Mke aliyetoka kwenye nafasi yake huanza kutaka nafasi ya mumewe na hasa kwenye kufanya maamuzi ya mwisho. Hivyo hutaka akisema yeye mumewe asiongezee lolote ndo atajiona kupendwa na kutahaminiwa na hii haimaanishi mke we zezeta hapana ila kuna maamuzi lazima KIONGOZI aseme,maana makamu wa rais hawezi kuwa rais katika hali ya kawaida.
The same kwa mume.

Mwana mpotevu alipotoka kwenye nafasi yake,hakuna alichofurahia na akiwe nje ya nafasi yake asingesikiwa maombi mengine yoyote mpaka alipoomba TOBA,KUGEUKA.
Hata uwe na elimu kuliko mumeo,bado wewe ni msaidizi mwenye hela kuliko kiongozi.
Hata uwe na akili kuliko mumeo,bado wewe ni msaidizi mwenye akili kuliko kiongozi wake.
Swala la NAFASI halibadilishwi kwa elimu au cheo au pesa...lilishwekwa hivo.
Mnalifahamu lile andiko linaonyesha kuwa maombi ya mume, kujibiwa kwake na Mungu inategemea anavyoishi na MSAIDIZI WAKE?
Eva asingekuwa KIONGOZI kwa kujifanya mjuaji.

1 Peter 3:7 tusome
7 Kadhalika ninyi waume, ishini na wake zenu kwa kuwahurumia, mkitambua ya kuwa wao ni dhaifu na hivyo muwape heshima, kwa maana ninyi ni warithi pamoja nao wa neema ya uzima.

Fanyeni hivyo ili sala zenu zisizuiliwe.
Je, tunajua kuwa NAFASI ya USAIDIZI ya mwanamke ndiyo hiyo hiyo nafasi ya USAIDIZI ya ROHO MTAKATIFU?

Quotes by Raphael JL: Kujisahaulisha hali ulonayo hakuiondoi hiyo hali. Kubali kuwajibika,hakuna malaika atakuja kukutoa kwenye hali yako kama hauko tayari. Njia rahisi na pekee ya kuukwepa ujinga ni kujifunza. CHOOSE TO BECOME.
Ushirika na Mungu!

Usikate tamaa
Usirudi nyuma
Usiache unachofanya
Usikimbie kazi
Usijichukie
Usijihurumie
Usikubali kudharauliwa kwasababu yoyote ile
Usikubali kuonekana huna maana
Usikubali kuonekana hufai
Mkono mwema wa Bwana ukusaidie
Nakataa kuonewa juu yako
Nakataa kuonewa juu ya familia na uzao wako
Nakataa kuolewa kazini kwako
Naakataa kuonewa kwenye biashara yako
Hakuna wa kukutoa kweney nafasi yako
Hakuna wa kukuonea mbele yako
Usikubali kutoka kwenye nafasi yako
Usikubali kuacha wajibu wako
Usicahe shule
Usiache ndoa yako
Kama unajua hujakosea, usiache....kama unajua umekosea basi tubu
Ugumu haimaanishi haiwezekani
Kaa kwenye nafasi yako
Maombi yanayojibiwa nje ya nafasi ni maombi ya toba tu
Unahama unaenda wapi?
Mungu akurejeshee furaha yako
Mungu akurejeshee tumaini
Mungu akurehemu na kukufanyia wepesi
Usiache bana.
Usikimbie
Kimbia kama unajua umemaliza wajibu
Wengine wanakimbiza pesa wanamuacha mungu bado amekaa anakunywa kahawa
Wengine wanakimbiza umaarufu na kujulikana
Nakusihi mwana wa Mungu
Usikurupuke
Furaha ya kweli iko kwenye nafasi yako
Kama ulimuomba mungu kupata hiyo kazi au hiyo biashara usiache kwa hiari yako-utateseka sana
Kumbuka ni wapi ulipokosea, rudi hapo ukaweke mambo sawa
Mungu akutokeeeee
Usiende kwengine bila Mungu
Usiende peke yako
Usikimbie bila Mungu
Umemuacha Mungu wapi?
Furaha na amani iko kwake, ukiwa nae unafurahia
Kila ulichokipata pamoja na mungu usikiache kwa akili zako mwenyewe au mazingira
Ulipokosea ndo penye jibu-kubali kuwajibika
Ipo njia ionekanayo kuwa sawa machoni pako ila imebea uharibifu ndani yake
Stay in your position



ITAENDELEA...

Maoni 1 :

  1. Asante sana Mwalimu. MUNGU azidi kukupa Hekima. Kwa kweli kmepona. Na Yesu ansaidie kuyaishi haya nlojifunza.

    JibuFuta

Inaendeshwa na Blogger.